http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

CHADEMA yatoa tamko kumuombea Lissu kesho


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Baraza la vijana CHADEMA (BAVICHA) limewataka watanzania wote kwa ujumla hasa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kujitokeza siku ya kesh...

VIDEO: Mahakama ya Tanzania yaidhinisha umri halisi wa kuolewa kwa mtoto wa kike.
Mapigano makali yaibuka nchini Sudani......!!!!
Waziri Muhongo : Serikali Ya Uganda Kujenga Kiwanda Cha Kuchakata Mafuta Ghafi Na Kuwa Safi
Baraza la vijana CHADEMA (BAVICHA) limewataka watanzania wote kwa ujumla hasa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kujitokeza siku ya kesho (Jumapili) katika maombi ya Tundu Lissu kwa madai wamekamilisha taratibu zote za kisheria juu ya jambo hilo.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu (BAVICHA) Taifa, Julius Mwita kupitia ukurasa wao maalum wa Facebook wa chama hicho baada ya siku ya jana Kamishna Kanda maalumu ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa kuzuia kufanyika kwa maombi hayo.

"Kupitia kamati ya maandalizi, BAVICHA inapenda kuwaambia Watanzania wote ambao watapenda kuhudhuria maombi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kuwa maandalizi yote muhimu yameshafanyika kwa ajili ya kuhakikisha shughuli hiyo ya kiimani inafanyika kama ilivyopangwa", amesema Mwita.

Julius Mwita aliendelea kwa kusema mpaka sasa wameshafuata taratibu zote za kisheria ambazo zimewaelekeza kutoa taarifa kwa mamlaka za kiserikali hususani Jeshi la Polisi
"Hadi sasa jeshi hilo halijatuandikia barua ya kutuita ili kujadiliana nao kuhusu kufanikisha shughuli hiyo, tunaamini kuwa hawana pingamizi lolote la kiutaratibu kama ambavyo sheria inaelekeza. Tumefuatilia kwa kina kuhusu kauli za Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa ambazo zimenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari leo ikidhaniwa kuwa amezuia shughuli hiyo ya maombi, na tumebaini kuwa ZPC Mambosasa hakueleweka vyema", amesema Mwita.

Pamoja na hayo, Mwita ameendelea kwa kusema "Tumejiridhisha tena kuwa taarifa tuliyopeleka kwa jeshi la polisi kama sheria inavyoelekeza, tukiwataarifu kuhusu maombi hayo, haikutaja wala kuzungumzia maandamano bali watu wa dini mbalimbali zilizopo nchini wanaoguswa na tukio la Lissu na maumivu anayopitia hospitalini, watakutana na kuomba sala au dua ili Mwenyezi Mungu afanye uponyaji kwa mgonjwa wetu", amesisitiza Mwita.

Kwa upande mwingine, Katibu Mkuu (BAVICHA) Taifa, Julius Mwita amesema maombi hayo yatafanyika kesho (Jumapili) katika uwanja wa Tip, Sinza darajani jijini Dar es Salaam kuanzia majira ya saa 8:00 mchana.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : CHADEMA yatoa tamko kumuombea Lissu kesho
CHADEMA yatoa tamko kumuombea Lissu kesho
http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2017/09/16/CHADEMAA.jpg?itok=eGRmeCuH×tamp=1505572491
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/chadema-yatoa-tamko-kumuombea-lissu.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/chadema-yatoa-tamko-kumuombea-lissu.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy