http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Vyama 10 Vya Upinzani Vyaungana Kuupinga UKUTA Wa Chadema


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

VIONGOZI wa vyama vya siasa wanaounda Klabu ya Viongozi wamesema hawaungi mkono maandamano yaliyopangwa na Chama cha Demokrasia na Maend...

Ugonjwa wa Dengue umerejea nchini kwa upya
Mange Kimambi aibukia Tarime
Waziri Hoi hospitalini Alazwa kuokoa Maisha yake

VIONGOZI wa vyama vya siasa wanaounda Klabu ya Viongozi wamesema hawaungi mkono maandamano yaliyopangwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika kulinda amani ya nchi.


Mwenyekiti wa klabu hiyo, Fahmi Dovutwa alisema uamuzi wa kutounga maandamano hayo imefikiwa kwenye kikao cha viongozi wa vyama wa siasa wa klabu hiyo waliokutana jana kujadili hali ya siasa nchini.


“Vyama vya siasa tumekutana leo (jana) ili kufanya tafakari juu ya hali ya siasa nchini hususan tamko la Chadema la kufanya maandamano na hatimaye mikutano sehemu mbalimbali. Pia tumezingatia tamko lililotolewa na Serikali na Rais John Magufuli la kutaka amani ya nchi idumishwe, hivyo hatuungi mkono maandamano,” alisema.


Alisema pamoja na kutounga mkono, viongozi hao wanataka kufanyika kwa mkutano ambao utashirikisha vyama vyote vya siasa nchini ili kupata muafaka ambao utaepusha nchi kuingia katika malumbano na misuguano.


“Tarehe waliyopanga kufanya hayo maandamano ni maadhimisho ya Siku ya Majeshi Duniani kote, hivyo wanajeshi watakuwa na shughuli zao ambazo zinaweza kuleta taswira ya jeshi kuingilia maandamano, lakini jambo la msingi ni kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwa vyama vyote,” alisema Dovutwa.


Vyama vilivyohudhuria mkutano huo ni Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Alliance For Tanzania Farmers Party (AFP), Chama cha Democratic (DP), D-Makini, JAHAZI Asilia, Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD), United Peoples Democratic Party (UPDP), ADA-TADEA na Chama Cha Kijamii (CCK).


Hivi karibuni, Chadema ilitoa tamko la kufanya maandamano na mikutano nchi nzima katika kampeni waliyoiita Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (UKUTA).


Azma ya Chadema inakuja baada ya siku kadhaa za Jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano kwa sababu za kiusalama.


Hata hivyo, Rais Magufuli alipiga marufuku maandamano hayo kwa lengo la kutaka amani ya nchi idumishwe na kuelekeza mikutano ya hadhara ya wabunge walioshinda ifanywe kwenye majimbo yao.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Vyama 10 Vya Upinzani Vyaungana Kuupinga UKUTA Wa Chadema
Vyama 10 Vya Upinzani Vyaungana Kuupinga UKUTA Wa Chadema
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYOaIBeypKJ1vL0xif_s_yYqTXfEyIPoWHrRMT55KJpX113zx0e8FJOoycsi7J9_OvpEHFzkG1FaU-A0QLEg1_1tCxFA7dNEOnIpt09BvfluEefxHUxtqNXdyhxYrfBI3U4gsvUGkaNC0/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYOaIBeypKJ1vL0xif_s_yYqTXfEyIPoWHrRMT55KJpX113zx0e8FJOoycsi7J9_OvpEHFzkG1FaU-A0QLEg1_1tCxFA7dNEOnIpt09BvfluEefxHUxtqNXdyhxYrfBI3U4gsvUGkaNC0/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/vyama-10-vya-upinzani-vyaungana.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/vyama-10-vya-upinzani-vyaungana.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy