http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Kundi la Original Comedy Matatani Kwa Kuvaa Sare za Jeshi la Polisi Kwenye Sherehe ya Masanja Mkandamizaji


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

katika  siku za hivi karibuni, kumejitokeza  tabia kwa baadhi ya watu wakiwemo wasanii watu wengine mmoja mmoja kutumia mavazi yanayofa...

Mkurugenzi wa Facebook, Mark Zuckerberg Atiwa kikaangoni
Rais John Magufuli atengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa(NHC),
Amuua Mkewe na Kuificha Maiti Kwenye Mbuyu kwa Miaka 8
katika  siku za hivi karibuni, kumejitokeza  tabia kwa baadhi ya watu wakiwemo wasanii watu wengine mmoja mmoja kutumia mavazi yanayofanana na sare za Majeshi ya Ulinzi na usalama hapa nchini likiwemo Jeshi la Polisi katika shughuli zao za kisanii au katika kazi mbalimbali, Jambo ambalo ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za Nchi.

Kwa mujibu wa Sheria ya kanuni za makosa ya Jinai, sura ya 16 na  marejeo yake ya mwaka 2002,  kifungu cha 178 (1) na  (2) kinachozungumzia makosa dhidi ya sare za majeshi ya ulinzi na usalama,  kinabainisha wazi kuwa ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ambaye siyo mtumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama kuvaa mavazi yanayotumiwa au kushabihiana na sare za majeshi hayo  bila kibali kutoka kwa  Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kufuatia  kitendo kilichofanywa na kundi la kisanii la “ Original Comedy” kuvaa mavazi yanayoshabihiana na sare za Jeshi la Polisi, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam linachukua  hatua za kisheria dhidi ya wasanii hao.

Aidha Jeshi la Polisi nchini, linatoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia  mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na  majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini na atakayebainika hatutasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yake.

Jeshi la Polisi linatoa rai kwa wale wote wenye mavazi yanayoshabihiana na sare za majeshi ya ulinzi na usalama  kuzisalimisha mara moja katika vituo vya Polisi vilivyokaribu nao.

 Imetolewa na:
Advera John  Bulimba – Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP)
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Makao Makuu ya Polisi. 

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Kundi la Original Comedy Matatani Kwa Kuvaa Sare za Jeshi la Polisi Kwenye Sherehe ya Masanja Mkandamizaji
Kundi la Original Comedy Matatani Kwa Kuvaa Sare za Jeshi la Polisi Kwenye Sherehe ya Masanja Mkandamizaji
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhr60sew8yJ5p3moe14MQT9rByKP0MnQ3wXtQ0bMU2kRWSfLvzUpuYrjYBheS80a_WB7ci_cj5aEn7x4b04eWRhiI3z9FkvRt-kx3kkYbJLqdbSMNEW1zMCP81ZTX6PnJBR7tqrwr-KHJE/s640/SWE4555.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhr60sew8yJ5p3moe14MQT9rByKP0MnQ3wXtQ0bMU2kRWSfLvzUpuYrjYBheS80a_WB7ci_cj5aEn7x4b04eWRhiI3z9FkvRt-kx3kkYbJLqdbSMNEW1zMCP81ZTX6PnJBR7tqrwr-KHJE/s72-c/SWE4555.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/kundi-la-original-comedy-matatani-kwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/kundi-la-original-comedy-matatani-kwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy