http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Bunge la Afrika Kusini limeshindwa tena kumuondoa Rais Zuma


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Rais wa Afrika Kusini amenusurika kwa mara nyingine katika kura ya kutokuwa na imani naye iliyopigwa na bunge la nchi hiyo ambapo awamu ...

CHADEMA Wampa Kazi Mke wa Lowassa
Moto waua na kujeruhi
Vikosi vya Marekani vyaharibu ngome ya Al-Shabaab Somalia

Rais wa Afrika Kusini amenusurika kwa mara nyingine katika kura ya kutokuwa na imani naye iliyopigwa na bunge la nchi hiyo ambapo awamu hii ilikuwa ni ya tofauti kwani ilikuwa ni kura ya siri.


Rais Zuma kwa vipindi mfululizo ameshuhudia maandamano na kura za kutokuwa na imani zikipigwa kwa lengo la kumtaka ajiuzulu kutokana na tuhuma mbalimbali za rushwa na upendeleo zinazomkabili.


Kutokana na kura zilizopigwa jana na bunge la nchi hiyo, jumla ya kura hizo ni 384 huku waliosema hawana imani naye wakiwa 177, wenye imani wakiwa ni 198 na kura zilizoharibika ni 9.


Kwa mujibu wa matokeo hayo, Wabunge 40 wa chama tawala, ANC wamepiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma hivyo kutaka ang’atuke.


Viongozi mbalimbali wa ANC pamoja na wabunge wengine wa chama hicho, wametaka wabunge hao (40) wachukuliwe hatua za kinidhamu kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kukisaliti chama.


Muda mfupi baada ya bunge kutangaza matokeo hayo yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu, wafuasi wa Rais Zuma walionekana wakicheza na kuimba kwa furaha nje ya jengo la bunge wakisherehea ushindi huo.


Aidha, kwa upande mwingine imeripotiwa kuwa, fedha ya Afrika Kusini (Rand) imeporomoka kwa zaidi ya asilimia 1 baada ya kutangazwa kuwa Rais Zuma ameshinda kwenye kura hiyo.


ANC imempongeza Rais Zuma kufuatia ushindi huo huku kikisema kwamba, mara zote kimekuwa kikitoa makada wenye kuaminika katika nafasi za serikali.


Rais Zuma amepigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa zaidi ya mara 5 ambapo mara zote amefanikiwa kuruka kiunzi na kuendelea kusalia madarakani.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Bunge la Afrika Kusini limeshindwa tena kumuondoa Rais Zuma
Bunge la Afrika Kusini limeshindwa tena kumuondoa Rais Zuma
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjtZjOuatBlEYUohTgWRCaRddr3y75b3rfyRcxq-RPhlst2L3x4JoX57CwOgXTAEVcsb3oLmIZV8y2PZfFRgLfZb-FQPtpIgVGCXREUGg4FZDStg2z1_xQjfJ9x33teA5tShTpZ6LfNtEfM/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjtZjOuatBlEYUohTgWRCaRddr3y75b3rfyRcxq-RPhlst2L3x4JoX57CwOgXTAEVcsb3oLmIZV8y2PZfFRgLfZb-FQPtpIgVGCXREUGg4FZDStg2z1_xQjfJ9x33teA5tShTpZ6LfNtEfM/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/08/bunge-la-afrika-kusini-limeshindwa-tena.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/08/bunge-la-afrika-kusini-limeshindwa-tena.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy