http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Nyuki hatari wagundulika Dodoma


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Dodoma. Siku chache baada ya ofisa wa Ikulu, Frank Lyimo kufariki dunia baada ya kuumwa na nyuki, Manispaa ya Dodoma imebaini maeneo manne y...

BREAKING: Tangazo la Majina ya Watumishi wa Umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo ya Mishahara baada ya Uhakiki
Diamond Kortini Mahakama ya Kisutu
TANZIA;Tambwe kadà wa chadema ,Hizza afariki dunia


Dodoma. Siku chache baada ya ofisa wa Ikulu, Frank Lyimo kufariki dunia baada ya kuumwa na nyuki, Manispaa ya Dodoma imebaini maeneo manne yenye makundi ya nyuki ambayo ni hatari kwa binadamu.

Maeneo yaliyobainika kuwa na makundi ya nyuki ni Zahanati ya Makole, Dodoma Makulu, Kisasa na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).
Ofisa Nyuki wa Manispaa ya Dodoma, Vedastus Milinga alisema baada ya tukio la Lyimo kung’atwa na nyuki wakati akipita katika nyumba ya kulala wageni ya Formula One eneo la Makole mjini hapa, wamepokea taarifa za uwapo wa nyuki kwenye maeneo mengine.

“Sasa hivi nyuki wapo wengi mtaani kwa sababu wanatafuta mizinga. Hivyo wakazi wa mji huu wanatakiwa kutupatia taarifa wanapoona makundi ya nyuki ili tuwaondoe,” alisema Milinga.
Akizungumzia suala hilo Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Kanda ya Kati, Mathew Kiondo alisema baada ya kubaini uwapo wa nyuki wamemwagiza ofisa nyuki wa manispaa ya Dodoma kupeleka bajeti kwa ajili ya kuwaondoa.

Alisema tangu mwaka huu uanze kumekuwa na matukio matatu ya watu kufa kwa kuumwa na nyuki katika maeneo ya Hombolo, Makutopora na Makole.

“Tumeamua kuanza kutoa elimu kwa wananchi wajue umuhimu wa kutoa taarifa na kutoa huduma ya kwanza wakati

mtu anapoumwa na nyuki,” alisema.
Alifafanua kuwa watapitisha gari la matangazo na vipindi vya redio kutoa elimu hiyo.
Alipoulizwa kuhusu malalamiko ya Mwenyekiti wa Makole, Anne Ngaya kueleza kudaiwa gharama za kuondoa nyuki katika eneo lake, Kiondo alisema kazi ya TFS ni kutoa ushauri kwa ufugaji wa nyuki. “Hatuwezi kufahamu kuhusu uwapo wa nyuki bila kupata taarifa kutoka kwa wananchi au viongozi ambalo ni jukumu lao. Na hii operesheni ya kuondoa nyuki ina gharama zake ambazo ni lazima mtu atatakiwa kutoa kwa ajili ya kununulia dawa,” alisema.

Kiondo alisema majibu aliyoyapata Anne kuwa kuna gharama za kugharamia kazi hiyo ni sahihi kwa kuwa ofisi hiyo haipangi bajeti kwa ajili ya kuteketeza nyuki.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Nyuki hatari wagundulika Dodoma
Nyuki hatari wagundulika Dodoma
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3862824/highRes/1598380/-/maxw/600/-/jrmabh/-/BEEEES.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/nyuki-hatari-wagundulika-dodoma.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/nyuki-hatari-wagundulika-dodoma.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy