Watu wawili wamefariki dunia baada ya lori lililokua limepakia makaa ya mawe mali ya kampuni ya Full Cargo Support ku...
Watu wawili wamefariki dunia baada ya lori lililokua limepakia makaa ya
mawe mali ya kampuni ya Full Cargo Support kupinduka katika eneo la
Utwango wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma likitokea wilaya ya Mbinga
mkoani humo kuelekea jijini Dar es salaam.
Kamanda
wa polisi wa mkoa wa Ruvuma, SACP Gemini Mushy amewataja watu hao kuwa
ni Ahmad Rajab (47) aliyekuwa dereva wa lori hilo pamoja na Abiud Daudi
(25) aliyekuwa utingo wa lori hilo na amesema chanzo cha ajali hiyo ni
kutokana na mwendokasi wa dereva wa gari hilo iliyopelekea kushindwa
kumudu kona ya barabara hiyo na hatimaye kuacha njia na kupinduka eneo
la mtoni na kisha kupelekea vifo vyao papo hapo.
Kwa mujibu wa kituo cha Televisheni ya
ITV imesema kuwa imeshuhudia shughuli za uokoaji wa miili ya watu hao
zikiendelea kutokana na kubanwa vibaya na vyuma vya lori hilo aina ya
Daf lenye namba za usajili T 782 CMC na tela T 841 CLP mali ya kampuni
ya Full Cargo Sapport mara baada ya gari hilo kuacha njia na kupindukia
katika eneo hilo la Utwango wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma leo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Utwango wilaya
ya Namtumbo mkoani humo, Bw. Optatus Mapunda amesema eneo hilo limekuwa
likisababisha ajali mara kwa mara na kwamba mwezi uliopita lori mali ya
Dangote likiwa limepakia makaa ya mawe nalo lilipinduka.



