http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Mawakili Wambana Ester Bulaya Mahakamani....Vielelezo Idadi ya Wapiga Kura Vyatofautiana


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya jana alikaliwa kooni na mawakili wa wadai katika kesi ya kupinga matokeo ya uchagu...

MAMAKE TUPAC SHAKUR AAGA DUNIA
HALI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA
Leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya jana alikaliwa kooni na mawakili wa wadai katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi 2015 wakimtaka kutoa ufafanuzi wa idadi ya wapigakura waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.


Katika uchaguzi mkuu wa ubunge Jimbo la Bunda Oktoba 25, 2015, Bulaya alimbwaga mgombea wa CCM na mwanasiasa mkongwe, Stephen Wasira lakini wapigakura wanne walifungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga matokeo. Ester alikuwa mbunge wa viti maalumu CCM, lakini alihamia Chadema na kumshinda mkongwe Wasira.


Katika kesi hiyo ambayo vikao vyake vinafanyika mjini Musoma na ikiwa ni siku yake ya kwanza kutetea ubunge wake, Bulaya alibanwa na mawakili wa walalamikaji wanaopinga ushindi wake baada ya idadi ya wapiga kura iliyoandikwa kwenye kiapo chake kuwa tofauti na iliyoandikwa na msimamizi wa uchaguzi kwenye fomu namba 24B ya matokeo ya uchaguzi.


Bulaya alidai idadi ya wapiga kura walioandikishwa katika fomu ya matokeo namba 24B aliyopewa ilikuwa 69,369 lakini imetofautiana na aliyokuwa nayo msimamizi wa uchaguzi ambayo kuna jumla ya wapiga kura 69,460 baada ya kujumlisha kura zote.


Wakili wa upande wa mleta maombi, Hajra Mungula alitaka kujua kutoka kwa mbunge huyo idadi ipi sahihi kati ya ile aliyoandikiwa na msimamizi wa uchaguzi kwa mkono baada ya kuikataa ile ya kwanza na kutangaza idadi ya wapigakura wa wilaya nzima ya Bunda ambao ni 164,794 au ile iliyotangazwa na msimamizi huyo.


Mbunge huyo alidai kuwa wakati msimamizi anabadilisha idadi hiyo hakuona takwimu sahihi wakati anaandika kwa kuwa alikuwa amekaa mbali kidogo ila aliamini kilichokuwa kinaandikwa na msimamizi huyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Lucy Msofe


Wakili huyo alitaka kujua ilikuwaje hadi akaijua idadi hiyo ya wapiga kura wa wilaya nzima waliojiandikisha ambao ni 164,794 wakati hajui idadi ya wapigakura katika majimbo mengine ya wilaya hiyo? Mbunge huyo alijibu kuwa yeye aliifahamu idadi hiyo baada ya kupitia daftari la wapiga kura kabla ya uchaguzi kuanza.


Alidai alifahamu idadi hiyo kwa kuwa aliwahi kuwa diwani na alishakuwa kiongozi kabla ya kuwa mbunge na kusema kuwa taarifa za idadi ya wapiga kura kwa kawaida siyo siri.


Mbunge huyo alieleza kuwa tofauti ya idadi ya wapiga kura 69,460 na 69,469 haikuwa sawa lakini pia haikuathiri matokeo ya uchaguzi katika jimbo hilo wala kuathiri idadi yoyote ya wapiga kura kwa kuwa tofauti hiyo ni ndogo sana.


Alipohojiwa na wakili wa mleta maombi wa tatu Constantine Mutalemwa, “Ni nani aliyeziingiza takwimu hizo zinazopishana kwenye fomu namba 24B ya matokeo ya uchaguzi, Mbunge huyo alijibu kuwa aliyeingiza takwimu hizo kwenye fomu namba 24B ni msimamizi wa uchaguzi.


Mawakili wa upande wa Serikali ni Angela Lushagala na Michael Haule; Bulaya anatetewa na Tundu Lissu huku upande wa waleta maombi watatu mawakili ni Yasini Membe, Hajra Mwingula na Constantine Mutalemwa.


Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo chini ya Jaji Noel Chocha.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mawakili Wambana Ester Bulaya Mahakamani....Vielelezo Idadi ya Wapiga Kura Vyatofautiana
Mawakili Wambana Ester Bulaya Mahakamani....Vielelezo Idadi ya Wapiga Kura Vyatofautiana
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguUvr0VOM7JHfo7kQGn6_LHCED_QqSqPvp36jAbDv3rAh6eXlhuz0F_7_Pv_hzjnTCGJkKT4-AqdbtCDYni2K7gFzcU73Qwi7s6hufNYgWzi4t_NdsCEhNGF0GFDQCy8ShlT_wgtGavGQ/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguUvr0VOM7JHfo7kQGn6_LHCED_QqSqPvp36jAbDv3rAh6eXlhuz0F_7_Pv_hzjnTCGJkKT4-AqdbtCDYni2K7gFzcU73Qwi7s6hufNYgWzi4t_NdsCEhNGF0GFDQCy8ShlT_wgtGavGQ/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/mawakili-wambana-ester-bulaya.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/mawakili-wambana-ester-bulaya.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy