http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

JESHI LA POLISI MKOANI PWANI KWA KUSHIRIKIANA NA MAOFISA WA MALIASILI WAMEKAMATA VIROBA VIWILI VIKIWA VIMEJAA BANGI


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Askari polisi wa kituo cha polisi cha Chalinze akionesha viroba viwili vya bangi vyenye uzito wa kilo 50 kila kimoja vilivyokamatwa jana k...

Mtu Mmoja Akamatwa Akiingiza Nyama Zikiwa na Smart Phones 5 Kwa Wafungwa Gereza la Keko
VIDEO: “Ni vizuri ukweli huu ukasemwa” – Nape Nnauye
TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA




Askari polisi wa kituo cha polisi cha Chalinze akionesha viroba viwili vya bangi vyenye uzito wa kilo 50 kila kimoja vilivyokamatwa jana katika Operesheni ya kuthibiti utoroshaji wa mazao ya Misitu yasiyo na kibali katika kata ya Vigwaza tarafa ya Chalinze mkoani Pwani katika Bara bara kuu ya Morogoro wakitokea Tunduma wakiwa kwenye gari lenye namba za usajili T876 DDL aina ya DAF Leyland ( Picha na Lusungu Helela- Afisa Habari Maliasili na Utalii)



Viroba viwili vya bangi vyenye uzito wa kilo 50 kila kimoja vilivyokamatwa jana katika Operesheni ya kuthibiti utoroshaji wa mazao ya Misitu yasiyo na kibali katika kata ya Vigwaza tarafa ya Chalinze mkoani Pwani katika Bara bara kuu ya Morogoro vikitokea Tunduma vikiwa kwenye gari lenye namba za usajili T876 DDL aina ya DAF Leyland ( Picha na Lusungu Helela- Afisa Habari Maliasili na Utalii)



Kaimu mkuu wa Kanda ya Pwani wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Bw. Jonathan Mpangala akiwaonesha waandishi wa habari gari lililokuwa limebeba magunia mawili ya mkaa ambayo ndani yake kulikuwa na viroba viwili vilivyojaa bangi vyenye uzito wa kilo 50 kila kimoja ( Picha na Lusungu Helela- Afisa Habari Maliasili na Utalii)



Moja ya Kiroba kilichojaa bangi chenye uzito wa kilo 50 kilichokamatwa jana katika Operesheni ya kuthibiti utoroshaji wa mazao ya Misitu yasiyo na kibali katika kata ya Vigwaza tarafa ya Chalinze mkoani Pwani katika Bara bara kuu ya Morogoro kikitokea Tunduma kikiwa kwenye gari lenye namba za usajili T876 DDL aina ya DAF Leyland (Picha na Lusungu Helela- Afisa Habari Maliasili na Utalii)

………………………………………………………….

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maofisa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) inamshikilia Dereva Bw. Emanuel Bisama (37) ambaye ni mkazi wa Kimara Suka Dar es Salaam,kwa kosa la kusafirisha magunia mawili ya mkaa ambayo baada ya kupekuliwa ndani yake kulikutwa na viroba viwili vyenye uzito kilo 50 kila kimoja vikiwa vimejaa bangi.

Akizungumza jana na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Pwani , ACP. Bonaventura Mushongi alisema Mtuhumiwa ambaye ni dereva wa gari lenye namba za usajili T876 DDL aina ya DAF Leyland Bw. Emanuel Bisama (37) alikamatwa Septemba 21 saa 4.00 asubuhi katika kata ya Vigwaza tarafa ya Chalinze mkoa wa Pwani katika Bara bara kuu ya Morogoro akitokea Tunduma na kwa sasa yupo mbaroni kwa mahojiano licha ya kukana kuwa hakujua kilichomo ndani ya magunia hayo.

Kamanda Mushongi alisema walifanikiwa kumkamata wakiwa katika Operesheni ya Ukaguzi wa mazao ya Misitu katika Barabara kuu ya Morogoro hadi Dare Salaam, aliongeza kuwa Dereva huyo wa gari amefunguliwa kesi CHA/RB/3039/2016 kwa kosa la kupatikana na bangi

Kwa upande Wakala wa Hudumza Misitu Tanzania (TFS) Kaimu wa Kanda ya Pwani Bw. Jonathan Mpangala alisema kuwa Mtuhumiwa huyo amefunguliwa kesi ya pili yenye CHA/RB/5113/2016 kwa kosa la kumiliki na kusafirisha mazao ya misitu bila kibali kwa sheria ya misitu namba 14 ya 2012 kifungu 88 na 89.

Alisisitiza kuwa Operesheni ya kukamata usafirishaji wa mazao ya misitu bila vibali itakuwa ya kudumu baada ya kuona magari mengi hasa makubwa yakiwa yamepakiwa magunia ya mkaa kuanzia mawili hadi matano ambayo yamekuwa yakioneka waziwazi hata ukiwa barabarani namengi yakiwa hayalipiwa ushuru wa Serikali kuu na hata magari mengine yakiwa hayajalipiwa ushuru wa Halmashauri

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : JESHI LA POLISI MKOANI PWANI KWA KUSHIRIKIANA NA MAOFISA WA MALIASILI WAMEKAMATA VIROBA VIWILI VIKIWA VIMEJAA BANGI
JESHI LA POLISI MKOANI PWANI KWA KUSHIRIKIANA NA MAOFISA WA MALIASILI WAMEKAMATA VIROBA VIWILI VIKIWA VIMEJAA BANGI
http://fullshangweblog.com/home/wp-content/uploads/2016/09/poo1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/09/jeshi-la-polisi-mkoani-pwani-kwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/09/jeshi-la-polisi-mkoani-pwani-kwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy