http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

HALI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Ujumbe wa mabalozi , na maofisa wa ngazi za juu wa balozi za Umoja wa nchi za Ulaya (EU)   pamoja na Canada umefanya ziara ya kikazi kati...

Dk Shein hakuna wa kumuondoa madarakani
Msikilize, AUDIO: Lowassa amtaka Rais Dkt Magufuli kufuta kauli yake
Taarifa ya TANESCO kuhusu kuzimwa kwa mfumo wa LUKU nchi nzima

Ujumbe wa mabalozi , na maofisa wa ngazi za juu wa balozi za Umoja wa nchi za Ulaya (EU)   pamoja na Canada umefanya ziara ya kikazi katika Baraza la Habari Tanzania Jijini Dar es Salaam ambapo ulijadili hali
ya vyombo vya habari nchini Tanzania ikiwamo kufungiwa kwa magazeti mawili ya Kiswahili – Mwananchi na Mtanzania.

Ujumbe huo uliongozwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya , Filiberto C. Sebbregondi.
Masuala yaliyozungumzwa katika mkutano huo uliofanyika katika ofisi za MCT Oktoba 7, 2013 ni pamoja na hali ya sheria za vyombo vya habari nchini Tanzania na kuona kama zinakwaza uhuru wa habari, weledi kwenye vyombo vya habari na Baraza linafanya nini kuboresha uandishi wa habari.

Mkutano huo pia ulijadili kuhusu hali ya vitisho dhidi ya haki za kitaaluma za waandishi wa habari ikiwemo hata mauaji yakitolewa mfano wa mauaji ya mwandishi Daudi Mwangosi mwaka jana.

Kwa jumla mabalozi hao wanaunga mkono uhuru wa habari na wamesisitiza kuwa uhuru huo ni nguzo muhimu ya demokrasia.
Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, aliwaambia mabalozi hao kuwa , ” Hatusemi kuwa hakuna makosa katika vyombo vya habari. Lakini tunasema makosa haya yasichukuliwe kama ni uhalifu kwani kuna njia nyingi ya kuyashughulikia..

“ Inasikitisha kwamba wakati tunapata sifa nzuri kwamba serikali yetu inakuza uwazi na kwamba Rais wetu ana dhamira kubwa ya kuendesha serikali kwa uwazi , ghafla serikali inafanya maamuzi kinyume na sifa inayojijengea”, alisema.

Katika taarifa iliyotolewa na Umoja huo wa Ulaya kufuatia kufungiwa kwa magazeti hayo mawili, umeitaka serikali kuchukua hatua za kudumisha uhuru wa habari na kukuza haki ya kupata habari.

Umoja huo umeeleza katika taarifa hiyo kuwa vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kuendeleza majadiliano kama hatua ya msingi ya kutatua tofauti.

Mabalozi wengine waliokuwemo kwenye ujumbe huo ni Olivier Chave wa Uswsi, Lennarth Hjelmaker wa Sweden, Johnny Flento wa Demanrk, Sinikka Antila wa Finland, Luis Guesta wa Hispania, Koen Adam wa Ubelgiji na Jaap Frederiks wa Uholanzi.

Wengine ni Balozi wa Canada Patricia McCullagh, Tom Vens mwanadiplomasia wa EU , Claude Blevin wa Ubalozi wa Ufaransa,  Maire Matthews wa Ubalozi wa Ireland, Lise Stensrud wa Norway na Ofisa wa Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi (SDC) Marcelina Biro.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : HALI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA
HALI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA
http://www.mct.or.tz/images/KAJUx.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/hali-ya-vyombo-vya-habari-nchini.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/hali-ya-vyombo-vya-habari-nchini.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy