http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Uchaguzi wa TLS: Lissu apendekezwa kutetea Urais wake, ajengewa hoja mbili


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Rais wa sasa wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika TLS, Tundu Antiphas Mughway Lissu amependekezwa kutetea Urais wa chama hicho katika u...

Hatimaye Dk Mwaka ajisalimisha Polisi
Kitwanga Akutana Uso Kwa Uso na Rais Magufuli
Mgombea wa kiti cha ubunge aliyegoma kula ndani ya miaka 16

Rais wa sasa wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika TLS, Tundu Antiphas Mughway Lissu amependekezwa kutetea Urais wa chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi ujao jijini Arusha. Lissu ambaye amekuwa kwenye matibabu kwa muda sasa akitibu majeraha ya shambulio la risasi, alishinda kwa kishindo katika uchaguzi wa TLS mwaka jana.

Taarifa za kuaminika kutoka TLS zinadokeza kuwa Lissu anapigiwa chapuo na Mawakili wengi kwa mambo mawili:
Mosi, ni kutokana na kutekeleza mambo mengi kati ya yale aliyoyaahidi wakati akiomba kuchaguliwa kuwa Rais wa TLS. Mambo hayo ni pamoja na kuifanya TLS kurudi kwenye misingi na majukumu yake pamoja na kusimamia ujenzi wa Jengo la TLS uliosuasua kwa muda mrefu.

Mambo mengine aliyoyaahidi na kuyatekeleza ndani ya mwaka mmoja wa Urais wake ni kupunguza au kuweka uwiano wa michango ya Mawakili huku Mawakili wakongwe wakitofautishwa na Mawakili wachanga. Tayari michango inatofautiana kati ya Wakili na Wakili kwa kuzingatia ukongwe. Tena, michango mingine imefanywa kuwa ni ya hiari.

Pamoja na kutokuwepo ofisini kwa muda mrefu, Lissu anatajwa kama mgombea (akipitishwa na Kamati ya Kuratibu Uchaguzi wa TLS) mwenye nguvu na asiyehitaji nguvu kubwa kujieleza au kuelezwa. Changamoto pekee itakuwa ni katika uwepo wake uchaguzini ingawa Mawakili wengi wameapa kumpigia kampeni na kumchagua kwa kishindo kikubwa hata asipokuwepo.

Sababu ya pili ya Lissu kupigiwa upatu ni kuwa Lissu ni mmoja wa Mawakili wenye uthubutu na anayeweza kuwasilisha maoni, mapendekezo na mawazo ya TLS kwa mamlaka yoyote bila woga, mawaa wala tatizo. Lissu pia ameiva katika lugha ya Kiswahili na Kiingereza ambazo ndizo hasa hutumika katika shughuli za kila siku za TLS.


chanzo........Jamiiforums

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Uchaguzi wa TLS: Lissu apendekezwa kutetea Urais wake, ajengewa hoja mbili
Uchaguzi wa TLS: Lissu apendekezwa kutetea Urais wake, ajengewa hoja mbili
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhzlFFfts7JKqt0-Q0aYAnUebnI8x38UtNozPIQWCTxUuzDM_LjYKBXgmOxvoASjovJDWOPBeUcIbLBaece1p526PaG4Kh7_3uyTWiWW9SMZJR9X5adI3bRT77pZiK-3VsVv2ySQRs5xxo/s1600/01.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhzlFFfts7JKqt0-Q0aYAnUebnI8x38UtNozPIQWCTxUuzDM_LjYKBXgmOxvoASjovJDWOPBeUcIbLBaece1p526PaG4Kh7_3uyTWiWW9SMZJR9X5adI3bRT77pZiK-3VsVv2ySQRs5xxo/s72-c/01.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/03/uchaguzi-wa-tls-lissu-apendekezwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/03/uchaguzi-wa-tls-lissu-apendekezwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy