http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Daladala mkoani Dodoma zagoma kwa kupinga manyanyaso

Zaidi ya mabasi 70 ya daladala yanayosafirisha abiria katika baadhi ya njia za manispaa ya Dodoma, yamegoma kutoa huduma kwa siku nzima ...



Zaidi ya mabasi 70 ya daladala yanayosafirisha abiria katika baadhi ya njia za manispaa ya Dodoma, yamegoma kutoa huduma kwa siku nzima ya leo kutokana na madai ya kunyanyaswa na askari wa usalama barabarani.


Daladala hizo zinazotoa huduma kati ya Jamatini na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) pamoja na Jamatini na Veyula, zilisimamisha huduma zake kwa siku nzima ya leo zikipinga manyanyaso ya askari hao.


Baadhi ya madereva wa mabasi hayo, wamesema wamechoshwa na manyanyaso kutoka kwa askari hao kwa vitendo vyao vya kuwakamata kiuonevu.


Wamesema sababu kubwa ya mgomo wao ni rushwa na manyanyaso wanayofanyiwa na baadhi ya askari hao wa usalama barabarani.


Hata hivyo, akijibu malalamiko ya madereva hao, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Dodoma, Marisone Mwakyoma, amesema sheria zipo wazi kama kuna mtu anaombwa rushwa na kutoa, wote wana makosa kwa sababu zipo ngazi za kuripoti matukio hayo.


Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) mkoa wa Dodoma, Conrad Shio, amesema baada ya kutokea kwa mgomo huo waliweza kutoa kibali kwa magari mengine kuweza kubeba abiria wasipate shida ya usafiri.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Daladala mkoani Dodoma zagoma kwa kupinga manyanyaso
Daladala mkoani Dodoma zagoma kwa kupinga manyanyaso
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiL0i7GOP1Npn5_qIun8taxm45KLTe8MF3T624g6OWh6a0lXjTPNx5WTsKABFOnMvL6Z_HA7CUtEnR_QRCsdTJMOHWSiDd5uLy0bfINF0f0Y1gNqiAlQLWTpumMmDyf7XpFmPEDFYtq5R8/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiL0i7GOP1Npn5_qIun8taxm45KLTe8MF3T624g6OWh6a0lXjTPNx5WTsKABFOnMvL6Z_HA7CUtEnR_QRCsdTJMOHWSiDd5uLy0bfINF0f0Y1gNqiAlQLWTpumMmDyf7XpFmPEDFYtq5R8/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/12/daladala-mkoani-dodoma-zagoma-kwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/12/daladala-mkoani-dodoma-zagoma-kwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy