http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Majambazi wateka basi, wapora madiwani


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAJAMBAZI sita wameteka basi la Kampuni ya Safi na likitokea Kijiji cha Mamba wilayani Chunya kwenda jijini Mbeya na kisha kuwapora abiria j...

BALAA JINGINE KWA LULU....KUPANDISHWA KIZIMBANI KESHOKUTWA KWA MAUAJI YA KANUMBA
Breaking News: WALIOFAULU USAILI KAZI ZA KISERIKALI -
Mama amuua mwanae kwa moto


MAJAMBAZI sita wameteka basi la Kampuni ya Safi na likitokea Kijiji cha Mamba wilayani Chunya kwenda jijini Mbeya na kisha kuwapora abiria jana.

Miongoni mwa waliotekwa ni pamoja na baadhi ya madiwani waliokuwa wakielekea mjini Chunya kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha Baraza la Madiwani Maalumu kwa ajili ya kupitia na kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika jana.

Akizungumzia tukio hilo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Ramadhani Shumbi aliyekuwa mmoja wa waathirika wa uvamizi huo, alisema tukio hilo lilitokea saa moja kasorobo asubuhi katika eneo la Loge.

Shumbi ambaye ni Diwani wa Kata ya Mamba, alisema walipofika eneo hilo lililo na msitu mkubwa, walikuta kuna gogo kubwa lililolazwa na kufunga barabara na kisha walijitokeza watu sita mmoja akiwa amebeba bunduki na wengine mapanga na fimbo.

Alisema watu hao walipiga risasi tatu hewani na kuanza kupiga vioo vya basi wakiwaamuru abiria washuke, lakini iliwachukua abiria takribani dakika 10 wakigoma kushuka kabla ya baadhi walioonekana kutishika zaidi kuanza kushuka kwa kuruka kupitia madirishani.

Alisema baadaye iliwalazimu abiria wote kushuka na ndipo jambazi wakaanza kuwasachi na kunyang’anya fedha taslimu na simu za mikononi huku walioonekana kubisha, wakipigwa.

“Baada ya kushuka tulilazwa chini na kuanza kukaguliwa ambapo walichukua fedha na simu na mimi mwenyewe ni mhathrika wa simu na fedha kidogo nilizokuwa nazo. Ushauri wangu ni kuwa mabasi kama haya yaanze safari saa moja asubuhi badala ya saa kumi na moja ama kumi na mbili,” alieleza diwani huyo.

Credity....Hbarileo

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Majambazi wateka basi, wapora madiwani
Majambazi wateka basi, wapora madiwani
http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/basi-overtake_210_120.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/08/majambazi-wateka-basi-wapora-madiwani.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/08/majambazi-wateka-basi-wapora-madiwani.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy