http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Masaburi Atajwa kama mtu aliyelianya jiji la Dar kuwa maarufu duniani


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo amekiri kuwa mtangulizi wake ambaye amefariki dunia, Didas Masaburi a...

Polisi wavamia mkutano wa Shekh Ponda
DC ARUSHA MJINI AWATAKA WANANCHI KUJIANDIKISHA VITAMBULISHO VYA TAIFA
BREKING NEWS.Raila Odinga ajiondoa kwenye uchaguzi mkuu Kenya



Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo amekiri kuwa mtangulizi wake ambaye amefariki dunia, Didas Masaburi alifanya kazi kubwa ya kuboresha miundombinu ya jiji hilo pamoja na kulitambulisha katika anga za kimataifa.


Meya Mwita ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam katika safari ya mwisho ya kuuaga mwili wa Marehemu Masaburi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.


“Binadamu anapokuwa ameondoka huwa tunazungumza mema aliyoyafanya katika jamii yetu. Mimi Sikuwahi kufanya nae kazi lakini nimekuta kazi ambazo amefanya katika halmashauri ya jiji,” amesema.


Ameongeza kuwa “Moja ya mambo ambayo sitasahau niliyoyakuta aliyoyafanya katika utawala wake ni kuuleta mradi wa DMDP uliolenga kusukuma na kutaka kuboresha maeneo ya miundombinu ya DSM, ukiona kazi aliyoacha mimi ndio naendelea nayo sasa.”


Amesema jambo lingine alilofanya Marehemu Masaburi enzi za utawala wake ni kuleta miji mikubwa duniani kuja kuwekeza na kutoa misaada ya kimaendeleo nchini.


Miongoni mwa majiji aliyoyataja Mwita ni jiji la Hamburg, Shanghai na Torotonto.


“Aliileta hapa miji mikubwa duniani, mimi napata mialiko sasa katika nchi mbalimbali na hii ni matunda ya jitihada zake katika kulitangaza jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.” amesema.


Pia Meya Mwita amesema kuwa, Masaburi alifanikiwa kutoa mamlaka na madaraka ya kiutendaji kutoka serikali kuu hadi serikali za mitaa.


“Alipokuwa akiongolea dhana kubwa ya kutoa madaraka kutoka serikali kuu kuja serikali za mitaahili, alikuwa anamaanisha. Jambo hili si jepesi kwa kuwa, halmashauri za mitaa bila ya kuwa na nguvu kubwa haziwezi leta maendeleo mfano Kenya na Uganda halmashauri zake zinauwezo na mamlaka ya kupanga maendeleo,” amesema.


Amesisitiza kuwa “Japo hakufanikiwa kwa kiwango hicho mawazo yake yataishi na mimi kama mrithi wake nitaendelea kuyaenzi.”


Marehemu Didas Masaburi enzi za uhai wake aliwahi kuwa Diwani wa Kata ya Kivukoni, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT).

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Masaburi Atajwa kama mtu aliyelianya jiji la Dar kuwa maarufu duniani
Masaburi Atajwa kama mtu aliyelianya jiji la Dar kuwa maarufu duniani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhC9j6gCzBkAE52eY1scYixbF-NfdI704soSE9K5vgEac5_sNzQbfErG1Aq3sWvTSz7mwUOkNiGlUD5lK1a0GVCfLx3xd8FjG9GCXdg9W7Hw10UFE-N4GwG7xIxy3ByWnrPl2d_875IbKM/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhC9j6gCzBkAE52eY1scYixbF-NfdI704soSE9K5vgEac5_sNzQbfErG1Aq3sWvTSz7mwUOkNiGlUD5lK1a0GVCfLx3xd8FjG9GCXdg9W7Hw10UFE-N4GwG7xIxy3ByWnrPl2d_875IbKM/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/masaburi-atajwa-kama-mtu-aliyelianya.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/masaburi-atajwa-kama-mtu-aliyelianya.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy