http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Mwanasheria TBC amruka Tido Mhando Mahakamani


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mwanasheria wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Gwakisa Mlawa, amedai mahakamani kwamba Bodi ya Wakurugenzi ya shirika hilo haikuj...

MBUNGE COSATO CHUMI AANZA KUTATUA TATIZO LA MAJI KWENYE SHULE ZA JIMBO LA MAFINGA MJINI
RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA MKUTANO WA 17 WA DHARURA WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
MKUU WA MKOA MGENI RASMI KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UTUME MKOA WA ARUSHA
Mwanasheria wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Gwakisa Mlawa, amedai mahakamani kwamba Bodi ya Wakurugenzi ya shirika hilo haikujua chochote kuhusu mkataba ulioingiwa kati ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu, Tido Mhando na Channel 2 Group Corporation (BV1).

Mlawa alidai pia mshtakiwa anayekabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh. milioni 887.1, aliingia mkataba huo bila baraka za bodi ya zabuni ya TBC.

Shahidi huyo wa pili alitoa ushahidi wake jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Leonard Swai, shahidi huyo alidai kuwa hakuwahi kuufahamu mkataba huo hadi alipopokea taarifa za kesi Juni, 2012 kutoka Channel 2 Group Corporation (BV1) kwamba TBC imekiuka mkataba wa kuwekeza mitambo ya digitali.

"Mheshimiwa hakimu mkataba huo ulisainiwa kati ya Tido na watu wawili wa Channel 2 Group Corporation (BV1). Pia kulikuwapo na nyongeza ya mkataba uliotiwa saini kati ya Juni, Agosti na Novemba mwaka 2008... TBC tulimwandikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kuomba ushauri naye aliagiza ateuliwe mwanasheria wa kimataifa ambaye ni mjuzi katika masuala hayo," alidai shahidi na kuongeza kuwa:

"Iliteuliwa kampuni ya uwakili ya Freshfield Bruckhaus Derringer us LLP ilikuja nchini TBC kufanya uchunguzi wa nyaraka na kwamba ililipwa malipo ya awali zaidi ya Sh. milioni 800...katika uchunguzi huo, ulibaini kuwa Tido alisababisha hasara ya fedha hiyo iliyokuwa kampuni ya uwakili," alidai Mlawa.

Alipohojiwa na wakili wa utetezi, Ramadhan Maleta, kama aliiona mikataba hiyo, shahidi alidai kuwa ilikuwa kama wameingia makubaliano ya awali ya maandalizi ya mchakato wa kuelekea kwenye digitali.

Katika kesi ya msingi, inadaiwa kuwa Juni 16, 2008, akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kutia saini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na channel 2 Group Corporation (BV1) bila kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Ununuzi na kuinufaisha BVl.

Katika shtaka la pili, Tido anadaiwa kutumia vibaya madaraka yake Juni 20, 2008 alipotia saini makubaliano kwa utangazaji wa digitali duniani kati ya TBC na BVl.

Katika shtaka la tatu, anadaiwa Agosti 11, 2008 na Septemba 2008 akiwa Dubai, Tido alitumia vibaya madaraka yake kutia saini mkataba wa makubaliano kwa ununuzi, usambazaji kufunga vifaa vya usambazaji na mnara wa utangazaji kati ya TBC na BVI na kuifaidisha BVI.

Katika shtaka la nne, anadaiwa kuwa Novemba 16, 2008 akiwa Dubai, Tido alitumia vibaya madaraka yake kutia saini mkataba wa makubaliano kwa kuendesha miundombinu ya utangazaji (DTT Broadcast Infrastructure) kati ya TBC na BVI na kuinufaisha BVI.

Katika shtaka la mwisho, anadaiwa kuwa kati ya Juni 16 na Novemba 16, 2008 akiwa UAE, Tido aliisababishia TBC hasara ya Sh. 887,122,219.19.

Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo ushahidi wa Jamhuri.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mwanasheria TBC amruka Tido Mhando Mahakamani
Mwanasheria TBC amruka Tido Mhando Mahakamani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiHEu3ACY4jRfHAmcfTpx_4ejZXUfP9CZOkZcndhqr31k65loWcFBqzRilKUE64YL7elT_yAGotO0GFs0DLeZSxEQjx_9AxnyoiJEB01U_k8X1VdPXX0xvSPVfFnvIo2Ja0JOHSktys8Noc/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiHEu3ACY4jRfHAmcfTpx_4ejZXUfP9CZOkZcndhqr31k65loWcFBqzRilKUE64YL7elT_yAGotO0GFs0DLeZSxEQjx_9AxnyoiJEB01U_k8X1VdPXX0xvSPVfFnvIo2Ja0JOHSktys8Noc/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/mwanasheria-tbc-amruka-tido-mhando.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/mwanasheria-tbc-amruka-tido-mhando.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy