http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Godbless Lema Awakumbuka Wafungwa....Amuomba Rais Magufuli Aingilie Kati la Wakili Mwale


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Leo  ikiwa ni sikukuu ya Krismasi, Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Godbless Lema amewatakia kheri wafungwa na mahabusu nchini. ...

Shambulio la bomu kwenye mabasi laua watu 126 Syria
Eka 17 za mashamba ya Bangi zafyekwa
Nape: Nikisema Ukweli naonekana Mkorofi, Ila haya Nimeyashuhudia Mwenyewe
Leo  ikiwa ni sikukuu ya Krismasi, Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Godbless Lema amewatakia kheri wafungwa na mahabusu nchini.

Lema ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) katika salamu alizotoa jana Jumapili Desemba 24,2017 amekumbusha kilichomtokea sikukuu ya Krismasi mwaka jana akitaka wenye mamlaka kusimamia haki kwa weledi.

‘’Wakati ninawakumbuka na kuwatakia heri ya Krismasi mahabusu na wafungwa wote nchini ni muhimu watu wote mlioko kwenye vyombo vya sheria mjue wajibu wenu, unapokosa utu na upendo maana yake ni kuumiza watu na kutesa watu mahali fulani,” amesema Lema.

Amesema, “Krismasi mwaka jana nilikuwa nimeshikiliwa kama mahabusu Gereza Kuu Arusha kwa kunyimwa dhamana, tukiwa gerezani mimi na wenzangu tulikuwa tunaandaa sikukuu ya Krismasi.”

Lema amesema anawakumbuka rafiki zake wengi aliokaa nao vizuri ambao wengine wamefungwa na baadhi bado wako mahabusu.

“Kwa kweli zaidi namkumbuka sana wakili Median Mwale ambaye amekuwa mahabusu kwa kipindi cha zaidi ya miaka sita. Ninamuomba Rais aingilie kati suala la Mwale, kwa kweli huyu mtu inatosha kuwepo magereza kwa zaidi ya miaka sita bila kuhukumiwa. DPP najua unajua watu wengi wako magereza, nguvu uliyopewa na sheria inapokosa upendo basi nguvu hiyo inakuwa ni ukatili,” amesema Lema.

Amesema Krismasi mwaka jana alikuwa gerezani baada ya ibada iliyoongozwa na Askofu Lebulu (Josephat - Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha) walifanya maandalizi ya kula chakula ambacho familia zao  ziliwapelekea.

“Tukiwa tunakula wakili Mwale alisema, Lema wewe utatoka na mimi na wenzangu namuomba Mungu Krismasi inayokuja niweze kuwa nje, kwa bahati mbaya wakili Mwale na rafiki zake bado wameshikiliwa gerezani.”

Amesema kwa kipindi alichokuwa gerezani ameelewa huzuni za familia na watuhumiwa, ndiyo sababu Rais alipowasamehe wafungwa na hasa wenye makosa makubwa alimshukuru kwa sababu anajua huzuni ya kukosa uhuru.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Godbless Lema Awakumbuka Wafungwa....Amuomba Rais Magufuli Aingilie Kati la Wakili Mwale
Godbless Lema Awakumbuka Wafungwa....Amuomba Rais Magufuli Aingilie Kati la Wakili Mwale
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinbIibxs0or8hIjmGnIPLi9t_Ubv5knkFkzcifsfIhWLtnxyrigxtgOYFfum0jCbi70rrn-HYFFnK-FWWoeOTP2vhKJvmYhqMIlFlOqRD7tyOhf4U0Wpjri2U1lE9dDoPLp1mKIiW3iZbl/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinbIibxs0or8hIjmGnIPLi9t_Ubv5knkFkzcifsfIhWLtnxyrigxtgOYFfum0jCbi70rrn-HYFFnK-FWWoeOTP2vhKJvmYhqMIlFlOqRD7tyOhf4U0Wpjri2U1lE9dDoPLp1mKIiW3iZbl/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/12/godbless-lema-awakumbuka.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/12/godbless-lema-awakumbuka.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy