http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

JESHI LA POLISI LAKAMATA WASIOJULIKANA WATANO DAR


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limetangaza kuwakamata watu watano ambao wamekiri kufanya uhalifu na kuvunja katika ofisi y...

Rais Magufuli avunja mamlaka Kigamboni
Maneno 20 kayaandika Lema baada ya Ofisi za Wakili wa Manji kuvamiwa
MC Pilipili amepata ajali, alazwa Bugando

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limetangaza kuwakamata watu watano ambao wamekiri kufanya uhalifu na kuvunja katika ofisi ya Mawakili ya Prime Atorneys iliyopo katika jengo la Prime house, Mtaa wa Tambaza, Upanga jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi limeweza kuwakamata watu hao ambao mwanzo baadhi ya wananchi walikuwa wakisema watu wasiojulikana ambao walifanya uhalifu huo na kudai wamekiri kuhusika na uvunjaji wa ofisi hiyo na kuiba.

"Kutokana na msako mkali jeshi la polisi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watano kuhusiana na kesi ya uvunjaji wa ofisi ya Mawakili ya Prime Atorneys mnamo Septemba 12, 2017 jeshi la polisi lilipokea taarifa ya kuvunjwa kwa ofisi ya mawakili hao ambapo wahalifu hao walifanikiwa kuvunja na kuiba kasiki iliyokuwa na pesa milioni tatu laki saba, waliiba kompyuta mpakato mbili pamoja na nyaraka mbalimbali za ofisi hiyo na wateja" alisema Lazaro Mambosasa

Aidha Kamanda Mambosasa aliendelea kusema kuwa kutokana na msako mkali uliofanywa na jeshi la polisi uliweza kuwakamata watu watano ambao waliwataja kuwa ni pamoja na "Said Idrisa Salehe (47), Mustapha Ibrahim Said (35), Somvi M Somvi (52), Imani Bago Mhina (36) na mshtakiwa na watano ni Husein Hajib Suleman (45) baada ya mahojiano na watuhumiwa hao wote wamekiri kuhusika na tukio hilo na kuonyesha Kasiki la fedha pamoja na mitungi mitatu ya gas iliyotumika kuvunja ofisi hiyo" alisema Mambosasa

Aidha Mambosasa amewataka Watanzania pamoja na viongozi mbalimbali kuwa wavumilivu pundu tukio linapotokea na kutoa nafasi kwa jeshi la polisi kuweza kufanya uchunguzi na upelelezi wake wa kina kuwapata wahalifu wanaokuwa wamehusika kwenye matukio hayo.


"Kwa hiyo masihara mengine yanayofanywa na Watanzania yanalenga kupotosha ukweli lakini pia wanajaribu kuingilia upelelezi wa polisi ili ukweli usijulikane sote sasa tunashuhuda tulianza kwa kutowafahamu mashuhuda lakini upelelezi wa kina umefanyika na tumewapata kwa majina na wao wenyewe wamekiri kufanya matukio hayo, sasa nimualike aliyekuwa akipotisha Watanzania kwa nguvu kuwa aliyetenda kosa hilo hajulikani aje sasa atueleze kuwa na yeye ni miongoni mwa waliotenda makosa hayo kwa sababu tayari hawa wapo na wamekiri kufanya makosa hayo" alisisitiza Mambosasa

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : JESHI LA POLISI LAKAMATA WASIOJULIKANA WATANO DAR
JESHI LA POLISI LAKAMATA WASIOJULIKANA WATANO DAR
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhL_GwQsU7JTrUAZwUTnb7Qr-f2v-bS2-IYN_A8DeVV79BngMJQloSVRZdxNdnRvsd7ykWOZ7pwr4cubq8P5EJVImGGcUxZhUCpOayqTtHVxI43aF5XhLp5mA5WkxxJ1VncLu2vZxuQkloT/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhL_GwQsU7JTrUAZwUTnb7Qr-f2v-bS2-IYN_A8DeVV79BngMJQloSVRZdxNdnRvsd7ykWOZ7pwr4cubq8P5EJVImGGcUxZhUCpOayqTtHVxI43aF5XhLp5mA5WkxxJ1VncLu2vZxuQkloT/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/jeshi-la-polisi-lakamata-wasiojulikana.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/jeshi-la-polisi-lakamata-wasiojulikana.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy