http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Rufaa ya Kesi ya Lema Agosti 6


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mahakama Kuu Agosti 16 inatarajia kusikiliza rufaa ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anayepinga kushtakiwa akituhumiwa kuhamasisha...

Mti wenye miaka 600 wapatikana nchini.
UPDATE:Mbunge Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana
Mjane aliyelalamika kwa JPM, 'ageuziwa kibao' aburuzwa kortini.

Mahakama Kuu Agosti 16 inatarajia kusikiliza rufaa ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anayepinga kushtakiwa akituhumiwa kuhamasisha maandamano yaliyopewa jina la Ukuta, Septemba Mosi mwaka jana.


Lema kupitia mawakili, John Mallya na Sheck Mfinanga anapinga kesi hiyo kusikilizwa katika mahakama za chini, akitaka Mahakama ya Katiba itafsiri kwanza vifungu vya Katiba na sheria ya vyama vya siasa.


Rufaa hiyo ilipangwa kusikilizwa jana na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Modesta Opio lakini iliahirishwa kutokana na kutokuwapo mahakamani mawakili wa Serikali, huku wa Lema wakieleza hawakuwa wamejiandaa kwa ajili ya usikilizwaji.


Lema katika kesi hiyo anadaiwa kuhamasisha kwa kutumia ujumbe wa WhatsApp maandamano ya Ukuta yaliyokuwa yamepangwa kufanyika Septemba Mosi mwaka jana nchi nzima.


Hata hivyo, yaliahirishwa na viongozi wa Chadema waliokuwa wameyaandaa.


Katika rufaa, Lema kupitia mawakili wake anaiomba Mahakama kutoa tafsiri ya ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria ya vyama vya siasa.


Mawakili hao wanaeleza Katiba na sheria hiyo inampa haki kiongozi au mwanasiasa, kufanya shughuli za kisiasa na si mtu mwingine kuwakataza au kuingilia kati.


Katika kesi namba 352/2016 , Hakimu Mkazi Bernard Nganga, Februari 8 alitoa uamuzi mdogo wa kutupilia mbali pingamizi la Lema la kutaka kesi hiyo iondolewe mahakamani hapo na kuhamishiwa Mahakama Kuu akisema kesi hiyo si ya kikatiba.


Hakimu Nganga wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha amesema kesi hiyo ni ya jinai na mahakama hiyo inaweza kuendelea kuisikiliza kwa mujibu wa sheria.

Lema alikata rufaa ambayo sasa itasikilizwa Agosti 16.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Rufaa ya Kesi ya Lema Agosti 6
Rufaa ya Kesi ya Lema Agosti 6
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjNPJrh4t7AGYQllGX-wMLogQYwgxm9bZ23X3O8iOwKMNQ9tnPS8ZuugcxyWDgC0fuGgtjH48XBk9zKxGriyrmnsSuyoKigHqwz15CiP0gqBl-ge-qpqjTsIZwYdTgN9NVAhJjrVv1iC9g/s640/lema.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjNPJrh4t7AGYQllGX-wMLogQYwgxm9bZ23X3O8iOwKMNQ9tnPS8ZuugcxyWDgC0fuGgtjH48XBk9zKxGriyrmnsSuyoKigHqwz15CiP0gqBl-ge-qpqjTsIZwYdTgN9NVAhJjrVv1iC9g/s72-c/lema.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/rufaa-ya-kesi-ya-lema-agosti-6.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/rufaa-ya-kesi-ya-lema-agosti-6.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy