http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Afya Kuhusu Uvumi Unaosambazwa Katika Mitandao ya Kijamii


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na Uvumi katika Mitandao ya Kijamii kuwa Serikali imeamua kushusha Mishahara ya Madaktari kwa asi...

Lowassa Akutana na Mbowe Kumpa Mrejesho wa Ikulu
Mtwara Wakesha Wakinywa Uji Baada ya mtoto kuzaliwa na Kuongea Papo Hapo
Angalia Makonda na DC Happy Walivyoweka Picha za Mbowe Hadharani
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na Uvumi katika Mitandao ya Kijamii kuwa Serikali imeamua kushusha Mishahara ya Madaktari kwa asilimia 30% ili kuendana na dhana ya Hapa kazi tu na kuwa Serikali   imekusudia kufuta malipo ya Posho za Wataalamu wa Afya walio katika Mafunzo kwa Vitendo .Ufafanuzi kwa Umma wa Watanzania na Watumishi wa Sekta ya Afya ni kuwa taarifa hizo siyo za kweli.

Taarifa aliyoitoa Katibu Mkuu (Afya) alipokuwa anaongea na Watumishi wa  Hospitali ya Bugando  ililenga kutoa ufafanuzi kwa Watumishi wa Hospitali hiyo kuhusu kufutwa kwa kibali cha Msajili wa Hazina kilichowawezesha  watumishi wa Hospitali hiyo kulipwa Mishahara ya Taasisi zilizo chini ya Msajili wa Hazina tangu mwaka 2012.

Uamuzi huo wa Msajili wa Hazina unatokana na ukweli kwamba Hospitali ya Bugando siyo Shirika la Umma na hivyo wanastahili kulipwa mishahara sawa na watumishi wengine wa Serikali Kuu kwa kuzingatia makubaliano yaliyopo kati ya Serikali na Baraza  la Maaskofu Tanzania  (TEC) ambao ndio wamiliki wa Hospitali ya Bugando.

Aidha, ieleweke kuwa mishahara ya Watumishi wa Sekta ya Afya haizingatii ngazi ya Vituo vya kutolea huduma kama vile Zahanati, Kituo cha Afya, Hospitali, au Hospitali za Rufaa bali huzingatia uzito wa kazi na majukumu ya kada husika. Hivyo, mshahara wa Daktari wa Hospitali ya Wilaya ni sawa na ule wa Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda.

Kutokana na maelezo haya, uamuzi huo wa Msajili wa Hazina utaihusu Hospitali ya Bugando pekee na siyo Hospitali zote za Kanda kwa kuwa dosari hiyo haikutokea katika Hospitali nyingine za Kanda.

Kuhusu ajira mpya kwa mwaka 2015/2016 ufafanuzi ulitolewa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba hakutakuwa na ajira mpya hadi hapo Zoezi la Uhakiki wa Watumishi Serikalini litakapokamilika.  Hivyo, vibali vya ajira vilivyokuwa vimetolewa vimefutwa hadi hapo itakapotamkwa vinginevyo.

Kadhalika, kumekuwa na Uvumi kuwa Serikali inakusudia kufuta posho ya ‘Interns' kuanzia mwaka huu wa fedha.  Taarifa hii pia siyo sahihi kwa kuwa hakuna chombo chochote cha Serikali ambacho kimetoa maamuzi hayo.

Wizara inasisitiza kuwa maamuzi ya Serikali hutolewa na Mamlaka husika  kwa nyaraka. Hivyo, watumishi wa Sekta ya Afya na wananchi kwa ujumla wanaaswa kuzingatia taarifa zinazotolewa na Mamlaka za Serikali kuhusu Masuala yanayowahusu ambayo mara nyingi hutolewa kwa nyaraka badala ya Mitandao ya kijamii,

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Afya
14 Julai, 2016

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Afya Kuhusu Uvumi Unaosambazwa Katika Mitandao ya Kijamii
Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Afya Kuhusu Uvumi Unaosambazwa Katika Mitandao ya Kijamii
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgh2u3fNA7_aVKv0pXhrwqDlhfXFy25BD0SIqmHhfRElET4qZOpop38M8O732XbN1LVmwNREcO4fPpBftbp07AYQFP5jB452hx5fYir3HrEeUDbm4Vkzs9BaFH9Z9v3VZYvBI0mKiC-Db0/s640/nembo.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgh2u3fNA7_aVKv0pXhrwqDlhfXFy25BD0SIqmHhfRElET4qZOpop38M8O732XbN1LVmwNREcO4fPpBftbp07AYQFP5jB452hx5fYir3HrEeUDbm4Vkzs9BaFH9Z9v3VZYvBI0mKiC-Db0/s72-c/nembo.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/taarifa-kwa-umma-kutoka-wizara-ya-afya.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/taarifa-kwa-umma-kutoka-wizara-ya-afya.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy