http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Wanafunzi kidato cha sita watakiwa kuepuka udanganyifu


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

WAHITIMU wa kidato cha sita wa shule ya sekondari Ruhuwiko katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wametakiwa kujiepusha kufanya vitendo ...

Sitta ahamishwa nyumba ya Serikali.....Awamu ya tano yagoma kumlipia kodi ya pango, Ahamia Mtaa wa Manzese
Marekani kuongeza wanajeshi Sudan Kusini
Mfanyabiashara Anayedaiwa Kujipatia Milioni 7 Kwa Dakika Afikishwa Mahakamani Na Kusomewa Mashitaka 199

WAHITIMU wa kidato cha sita wa shule ya sekondari Ruhuwiko katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wametakiwa kujiepusha kufanya vitendo vya udanganyifu kwenye mitihani.

Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani humo, Angelo Maskini alisema hayo alipokuwa akizungumza na wanafunzi, walimu na wazazi wakati wa mahafali ya 11 ya kidato cha sita katika shule hiyo, inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Brigedi ya Tembo.

Kwa mujibu wa Maskini, muda uliobaki kabla ya kufanya mitihani yao ni mdogo, kwa hiyo ni vema kuutumia kwa ajili ya kujikumbusha mambo ya msingi waliyofundishwa na walimu wao badala ya kuwa na mawazo mabaya ya kutamani kushiriki katika vitendo ambavyo vitawavunjia heshima na kukatisha ndoto zao.

Maskini alipongeza wahitimu hao kwa kufanikiwa kutimiza nusu ya ndoto walizonazo. Aliwataka kutoridhika na kiwango cha elimu walichonacho bali wawe na fikra na malengo makubwa ya kuendelea na elimu ya chuo kikuu ambayo inahitajika sana katika ulimwengu wa sasa.

Aidha, alikumbusha wazazi kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa kutoa ada na mahitaji mengine yanayohitajika kwa ajili ya watoto wao. “Wazazi wenzangu ni lazima sasa tubadilike tuache kutumia kiasi kikubwa cha fedha katika anasa, tujitahidi kutoa michango ya shule kwa ajili ya watoto wetu kwa muda muafaka ili wapate muda mwingi wa kujisomea,” alisema Maskini.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Brigedi ya 401 KV Tembo, Brigedi Kanali Iddi Nkambi amewataka wahitimu hao kwenda kuishi maisha ya kuiogopa zaidi dunia kama walivyokuwa wakiishi wakati wakiwa shuleni.

Nkambi ambaye pia ni Mkuu wa mafunzo na utendaji kivita, aliwataka vijana hao kuwa raia wema na kulinda nchi yao pamoja na kujiepusha kufanya vitendo vinavyoweza kuvuruga amani na upendo uliopo tangu uhuru.

Mkuu wa shule hiyo, Meja Paul Rugwaguza alisema, vijana hao walipokuwa shuleni walilelewa kwa nidhamu na kuandaliwa kuwa watu wema katika jamii. Rugwaguza alisema, shule hiyo ni kati ya shule bora ambazo zinafanya vizuri katika matokeo ya mitihani mbalimbali ya kujipima uwezo na hata ile ya kitaifa.


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Wanafunzi kidato cha sita watakiwa kuepuka udanganyifu
Wanafunzi kidato cha sita watakiwa kuepuka udanganyifu
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/wanafunzi-kidato-cha-sita-watakiwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/wanafunzi-kidato-cha-sita-watakiwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy