http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

MWANAFUNZI SUA AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMNYONGA


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamsaka mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Mwita Marwa (30) kwa tuh...

WALICHOKISEMA CHADEMA.baada ya Serikali kusema watagharamia matibabu ya Lissu
VIDEO,NAIROBI: TUNDU LISSU AKATWA MIGUU KWA MIKASI AKIWA CHUMBA CHA WATU MAUTUTI.
BREAKING: Serikali imesema iko tayari kugharamia matibabu ya Lissu
Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamsaka mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Mwita Marwa (30) kwa tuhuma za kumuua kwa kumnyonga mpenzi wake Kibua Adam (39) baada ya kutokea kutokuelewana kati yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema tukio hilo lilitokea Januari 22 mwaka huu katika eneo la Modeco Manispaa ya Morogoro ambapo mwanafunzi huyo alitoweka baada ya tukio hilo.
Amesema siku ya tukio mwanafunzi huyo na mpenzi wake ambaye ni mhudumu wa baa walichukua chumba katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kama Aluta ambapo walilala lakini baadaye mwili wa marehemu ulikutwa chumbani.
“Dada huyu mkazi wa Kihonda alikutwa ameachwa chumbani akiwa ameshafariki na baada ya uchunguzi ilionekana kwamba marehemu alinyongwa shingo kabla ya kifo chake,” amesema Kamanda Matei.
Hata hivyo, kamanda huyo amesema baada ya tukio hilo mtuhumiwa alimwandikia ujumbe wa simu dada wa marehemu aitwaye Happiness Adamu ujumbe akisema kwamba tayari marehemu keshatangulia na yeye mtuhumiwa atafuata.
“Nasikitika sana hamtatuona hapa duniani Mwita na Kibua, mimi ninayeandika meseji hii ni Mwita, nikimaliza nakunywa sumu au vidonge nife na mimi nimechoka na dunia na Kibua yeye keshatangulia, njooni hapa Aluta Bar mtutoe chumbani tulipolala,” ulisomeka ujumbe huo.
Hata hivyo, watu wa karibu wa marehemu ambao hawakutaka kutaja majina yao walisema marehemu alikuwa na mpenzi mwingine kabla ya Mwita na walipokorofishana ndipo alipoamua kuwa na Mwita lakini siku chache kabla ya tukio alimwambia Mwita kwamba mpenzi wake wa awali amejirekebisha hivyo anataka kurejeana naye jambo ambalo mtuhumiwa alikuwa analipinga.
Kamanda Matei amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Morogoro na jeshi hilo bado linaendelea na jitihada za kumsaka mtuhumiwa.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : MWANAFUNZI SUA AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMNYONGA
MWANAFUNZI SUA AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMNYONGA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg8LexSGoK7iXvDgN5l9rRKdTjePqOInkJicpbewxEBxxlNF_aGppux_-WOSb9-yp-UlbOjlFObyt3iFN2BNctjFVEanr2VwWYfJdZIk8hqB1761bym9-VNCGjiTrZovwaKp1ziIDID0eng/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg8LexSGoK7iXvDgN5l9rRKdTjePqOInkJicpbewxEBxxlNF_aGppux_-WOSb9-yp-UlbOjlFObyt3iFN2BNctjFVEanr2VwWYfJdZIk8hqB1761bym9-VNCGjiTrZovwaKp1ziIDID0eng/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/mwanafunzi-sua-amuua-mpenzi-wake-kwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/mwanafunzi-sua-amuua-mpenzi-wake-kwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy