http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Zitto Kabwe Apata Zigo....Mchage Ajivua Uanachama, Aachana na Siasa


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Aliyekuwa Katibu wa Bunge na Serikali za Mitaa katika Sekretarieti ya Chama cha ACT-Wazalendo, Habibu Mchange, amejiondoa uanachama wa ch...

Ubalozi wa Marekani nchini Kenya wafungwa baada ya Mtu Mmoja Kuuawa kwa Risasi Nje ya Ubalozi Huo
Tamko: CCM yawajibu Lowassa na Zitto Kabwe ..... Pia yakana kushiriki kwenye kuivuruga CUF
Sumaye: Sirudi CCM hata waninyang’anye Mashamba Yangu Yote

Aliyekuwa Katibu wa Bunge na Serikali za Mitaa katika Sekretarieti ya Chama cha ACT-Wazalendo, Habibu Mchange, amejiondoa uanachama wa chama hicho na kujiweka kando na siasa.


Taarifa ya uamuzi huo wa Mchange ilisambazwa jana katika mitandao ya kijamii, ikionyesha kuandikwa naye huku ikiambatanishwa na namba yake ya simu.


Katika andiko hilo, Mchange aliyewahi kuwa mwanachama wa Chadema kabla hajahamia ACT Wazalendo, alisema aliamua kujitoa rasmi katika ushiriki wa aina yoyote ya siasa ili apate muda zaidi wa kusimamia shughuli zake za kijasiriamali.


Mchange alisema ameamua kujiengua na siasa ili kutoa fursa na huduma sawa kwa viongozi na wanachama wa vyama vyote vya siasa.


“Kwa moyo mkunjufu kabisa na kwa mapenzi mema na taifa langu, ninathibitisha kwamba nimejitoa rasmi katika ushiriki wa aina yote ya siasa ili nipate muda mwingi zaidi kufanya na kusimamia shughuli zangu za kijasiriamali zinazonitaka nitoe fursa na huduma sawa kwa viongozi na wanachama wa vyama vyote vya siasa,” alisema Mchange.


Alisema kutokana na uamuzi huo ambao aliomba uheshimiwe, lolote atakalolifanya lisihusishwe na chama bali iwe ni msimamo wake mwenyewe kama mtu huru asiye na chama.


“Ninafahamu kuwa mwanachama wa chama cha siasa ni haki yangu ya kikatiba, lakini nimeamua kuihifadhi kwa sasa mpaka hapo nitakapoona inafaa kufanya vinginevyo. Ninawatakia kila la heri waliokuwa wanachama wenzangu wa ACT Wazalendo katika kuyafikia malengo ya msingi ya uanzishwaji wa chama hicho,” alisema Mchange.


Mchange alisema kujiondoa kwake kusihesabiwe kama sehemu ya kukwamisha au kurudisha nyuma matarajio na au malengo ya chama hicho bali ichukuliwe kama chachu ya kufika mbali.


“Msivunjike moyo, msirumbane, pendaneni, heshimianeni na shikamaneni ili mfikie lengo. Nitabaki na kuendelea kuwa ndugu yenu, rafiki na swahiba. Zaidi Mtanzania mwenzenu. Tutaendelea kushirikiana katika mambo yote ya kijamii na kimaisha yasiyohusiana na mlengo wa kiitikadi wa kisiasa,” alisema Mchange.


Mchange alishika nafasi mbalimbali katika chama hicho ikiwamo Katibu wa Mipango na Mikakati, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu.


Mchange anakuwa mwanasiasa wa tatu kuondoka ACT-Wazalendo mwaka huu baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Samson Mwigamba kuachia nafasi yake na kwenda masomoni nchini Kenya, Aprili mwaka huu.


Miezi michache baadaye, Novemba mwaka huu mwanasiasa Moses Machali naye alitangaza kujiondoa rasmi chama hicho na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dk. John Magufuli.


Machali aliwahi kuwa Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi kabla ya mwaka jana kushindwa kutetea jimbo lake kupitia ACT-Wazalendo.




Kutoka kwa HABIBU MCHANGE.

TAARIFA KWA UMMA
--------------------------------------
YAH:- KUJIVUA UANACHAMA WA ACT WAZALENDO NA KUTOSHIRIKI SIASA.... See More

304 24


source of information..Mpekuzihuru

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Zitto Kabwe Apata Zigo....Mchage Ajivua Uanachama, Aachana na Siasa
Zitto Kabwe Apata Zigo....Mchage Ajivua Uanachama, Aachana na Siasa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgx_BY9To1830_eHAOvpXgjU6Ql5P-_AqY9NGAnaFr-NHtCL3G8lxfrRsdStS8amHZ7lw85xO5hXsr_dDggadcxnAsGseEDgIecueH_QZt5w4AVbB9UMoYrhZTQ1wBDo6sIhgAlizrv_C8/s640/2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgx_BY9To1830_eHAOvpXgjU6Ql5P-_AqY9NGAnaFr-NHtCL3G8lxfrRsdStS8amHZ7lw85xO5hXsr_dDggadcxnAsGseEDgIecueH_QZt5w4AVbB9UMoYrhZTQ1wBDo6sIhgAlizrv_C8/s72-c/2.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/12/zitto-kabwe-apata-zigomchage-ajivua.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/12/zitto-kabwe-apata-zigomchage-ajivua.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy