http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Joseph Mungai Kuwagwa Leo Dar..........Mwili wa Samwel Sitta Kuwasili Leo


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Elimu, Joseph Mungai unatarajiwa kuagwa Dar es Salaam leo katika viwanja vya Karimjee. Akizungumza na w...

Katumbi asema atarejea DR Congo kuwania urais
MKURUGENZI ARUSHA AFAFANUA TUHUMA ZA UBADHIRIFU WA JENGO LA UTAWALA KALIUA
JENGO LA CWT PWANI ,LAIBIWA COMPUTER 11 NA ZAIDI YA MIL.5

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Elimu, Joseph Mungai unatarajiwa kuagwa Dar es Salaam leo katika viwanja vya Karimjee.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, mtoto wa marehemu, William Mungai alisema ibada ya kuuaga mwili huo itafanyika katika viwanja hivyo saa 5.00 asubuhi.


Hata hivyo mtoto huyo wa marehemu hakutaka kuingia kwa undani kuhusu chanzo cha kifo cha baba yake, badala yake alisema familia iachwe iendelee kushauriana na daktari.


Alisema pamoja na hayo, kifo hicho kimewashtua kwa vile kimetokea ghafla na kwamba baada ya kuisha kwa ibada ya kuaga mwili huo, utasafirishwa hadi Mafinga, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa kwa mazishi.


“Hadi sasa familia tunajua kwamba marehemu aliugua tumbo la kawaida na tulimpeleka hospitalini ambako alifariki dunia, tunaomba familia iachwe, kwa sababu bado tunashauriana na daktari wake.


“Tumekubaliana mwili wake uagwe kesho (leo) saa tano Viwanja vya Karimjee ambako pia historia yake yote na familia itasomwa,” alisema William.


Kifo cha Mungai kilitokea juzi jioni katika kile kilichoelezwa kuwa alianza kujisikia vibaya baada ya kunywa kiywaji katika hoteli moja iliyopo Msasani, ambayo aliizoea.


Mmoja wa waombelezaji waliofika nyumbani kwa marehemu jana ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)- Zanzibar, Salum Mwalimu ambaye alimwelezea Mungai kuwa aliunga mkono mabadiliko ya siasa.


“Hakuwa na kadi ya Chadema lakini alipenda mabadiliko, mwanaye William aligombea ubunge wa Mafinga kupitia Chadema na baba yake alimuunga mkono,” alisema.


Mbunge wa zamani wa Kwela, Chrisant Mzindakaya alisema amesikitishwa na kifo hicho ikizingatiwa wiki iliyopita walikuwa pamoja na walizungumza mambo mengi ya siasa.


“Hakuwa na kesho katika maisha yake, alilokuwa na uwezo wa kulifanya alilifanya siku hiyo hiyo, alikuwa na msimamo, hakukubali kuyumbishwa,” alisema Mzindakaya.


Wakati huohuo, mwili wa aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta unatarajiwa kuwasili leo ukitokea Ujerumani ambako alikuwa akitibiwa hadi mauti yalipomfika.


Taarifa zilizotolewa na msemaji wa familia ya marehemu, Gerald Mongella, zinasema mwili huo utawasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere saa 9.00 mchana na kupelekwa nyumbani kwake Msasani, Dar es Salaam.


“Ijumaa(kesho) saa tatu asubuhi ibada ya kuuaga mwili huo itafanyika katika viwanja vya Karimjee ambako ndugu na wakazi wa Dar es Salaam watapata fursa ya kuaga,” alisema Mongella.


Mwili wa Sitta utasafirishwa hadi Dodoma ambako utaagwa na wabunge na baadaye utasafirishwa kwenda Urambo kwa mazishi Jumamosi.


Sitta alifariki Novemba 07 mwaka huu katika Hospitali ya Technal University alipokuwa akipatiwa matibabu ya maradhi ya saratani ya tezi dume.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Joseph Mungai Kuwagwa Leo Dar..........Mwili wa Samwel Sitta Kuwasili Leo
Joseph Mungai Kuwagwa Leo Dar..........Mwili wa Samwel Sitta Kuwasili Leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhWDTHUXlX9Wvw8A38BYQ0GY3KoCrdibol1i66SBo6ljiCDIvlF3moSCPbo77PT2PL13a4Q7VvgN2xwXjJVKD9wisEO2PVWQ_28TfRzI6fafOXQEVWEsG-h0moHdTtDEWFsxaso3WO1vTg/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhWDTHUXlX9Wvw8A38BYQ0GY3KoCrdibol1i66SBo6ljiCDIvlF3moSCPbo77PT2PL13a4Q7VvgN2xwXjJVKD9wisEO2PVWQ_28TfRzI6fafOXQEVWEsG-h0moHdTtDEWFsxaso3WO1vTg/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/11/joseph-mungai-kuwagwa-leo-darmwili-wa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/11/joseph-mungai-kuwagwa-leo-darmwili-wa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy