http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

UKAWA. HII SASA DHARAU

  MGONGANO wa kiutawala umeanza kufukuta katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam, anaandika Happiness Lidwino. Cha...

 
MGONGANO wa kiutawala umeanza kufukuta katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam, anaandika Happiness Lidwino.

Charles Kuyeko, meya wa manispaa hiyo ameeleza kwamba, hayuko tayari kuona viongozi wanaotokana na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanakiuka mipaka ya taratibu za kazi kwa sababu za kiitikati ama dharau.


Meya huyo anayetokana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) amesema, hatua ya Isaya Mgurumi, mkurugenzi wa halmashauri hiyo alilotoa juzu kuwatimua wafanyabiashara wamachinga mjini bila kufuata taratubu inaonesha dharau.
Amesema, Mgurumi amefanya hivyo bila kumuhusisha meya na madiwani wa manispaa hiyo. Kutokana na kutishirikishwa kwao, leo wametengua uamuzi wa mkurugenzi huyo.

Katika kikao cha dharura kilichoitishwa leo na meya huyo, madiwani wa CCM hawakuhudhuria ambapo waliohudhuria ni madiwani kutoka kwa vyama upinzani.
Madiwani hao wamewataka wamachinga kutoondoka katika maeneo yao hadi watakapotafutiwa maeneo manzuri ya kufanyia biashara, huku wakimtaka mkurugenzi kurudi mezani kwa ajili ya mazungumzo.

Mgurumi juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, aliwataka wamachinga waliopo maeneo ya mjini hususan barabarani kuondoka mara moja ndani ya siku tatu.

Pia aliwapangia maeneo ya kwenda kufanyabiashara zao ambayo ni Ukonga Magereza, Muslimu Tabata, Kigogo Fresh na Kivule huku akiwatisha kwamba, atakayekaidi tamko hilo, mgambo na askari wa mabomu watafanya kazi yake.

Akizungumza na waandishi leo ofisini kwake Kuyeko amesema, amesikitishwa na tamko hilo ambalo hakushirikishwa kama kiongozi wa manispaa hiyo.

Amesema, badala ya kushirikishwa, aliletewa tamko hilo ili kutolea msisitizo.
“Nashindwa kuwaelewa viongozi wenzetu kwa kushindwa kutushirikisha masuala ya maendeleo katika manispaa tunayoiongoza wote.

“Yaani baada ya kufanya uamuzi na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa basi sisi wengine ambao tupo kwa niaba ya wananchi tunaonekana hatuna maana tena.
“Baada ya kutoa tamko ndio naambiwa nitoe msisitizo, hiyo ni dharau na ndio maana sikufanya hivyo,” amesema Kuyeko.

Amesema, licha ya yeye kutopewa taarifa hata madiwani wa maeneo ambayo mkurugenzi amewataka wamachinga kwenda hawana taarifa juu ya ugeni huo na kwamba, maeneo ya masoko hayatoshi kubeba watu wengi.

Patrick Assenga, Diwani wa Kata ya Tabata anasema, ameshangazwa na hatua mkurugenzi kufanya uamuzi kabla ya kuzungumza na viongozi wa maeneo husika.

“Hapa katika kata yangu soko halina vyoo wala maji ya kutosha, hata hivyo eneo ni finyu kutokana na kuwepo kwa shughuli nyingi za CCM ikiwepo ofisi yake na maegesho ya magari yao ambapo tumepiga kelele kwa muda mrefu waondoe shughuli zao lakini hadi sasa wamekaidi halafu wanaleta habari hizi,” amesema.

Stevene, Msigwa Mwenyekiti wa Wamachinga Wilaya ya Ilala amesema kuwa, wafanyabiashara hawana imani tena na serikali kwa kuwa, licha ya kushirikiana katika mambo mengi lakini imeamua kuwachukulia hatua kwa vitisho pasipo kuwashirikisha kwenye uamuzi huo.

“Ni vema wangetuita tufanye mazungumzo kabla ya kutuchukulia hatua kwani sisi ni binadamu na tuna majukumu, kuhamisha biashara kunahitaji maandalizi.

“Hatukaidi kuondoka ila hatutaondoka hata watumie mabomu hadi pale watakapotupatia maeneo manzuri yenye miundombinu mizuri kwani tunalipa kodi zetu,” amesema Msigwa.
Hata hivyo, madiwani waliohudhulia kikao hicho cha dharura wamesema, hawaina imani tena na mkurugenzi kutokana na maamuzi yake yasiyo shirikishi ambayo yanaonekana kuwa na shinikizo kutoka kwa Makonda.

Pia wamesema, endapo kesho shughuli hiyo itaendelea, watachukua hatua kali kutokana na kutosikilizwa.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : UKAWA. HII SASA DHARAU
UKAWA. HII SASA DHARAU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhI5lTf0IrHdSPW91OpZvIu6Ih-JbyXjvzdhMATFfcK4jd7RvdY2wZm9Bs1_OOASi14psLBldHF72UDsxiaT149dnZPBL0rbVmI3BgM8Qo5SJgsDD0qaq17P64xV3v8PKH5nAWvymU_IW_D/s640/DSC_0046.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhI5lTf0IrHdSPW91OpZvIu6Ih-JbyXjvzdhMATFfcK4jd7RvdY2wZm9Bs1_OOASi14psLBldHF72UDsxiaT149dnZPBL0rbVmI3BgM8Qo5SJgsDD0qaq17P64xV3v8PKH5nAWvymU_IW_D/s72-c/DSC_0046.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/ukawa-hii-sasa-dharau.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/ukawa-hii-sasa-dharau.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy