http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Mtuhumiwa kesi ya Mwangosi akana Ungamo Lake Mahakamani


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Chanel Ten mkoani hapa, Daudi Mwangosi, Pacificus Simoni ametoa ushahidi wake ...

Serikali yaanza upya kuhakiki vyeti feki
Matonya amekamatwa na madawa China ?
List ya Wabunge wenye kesi Mahakamani. Wako 13.

Mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Chanel Ten mkoani hapa, Daudi Mwangosi, Pacificus Simoni ametoa ushahidi wake mbele ya mahakama na kuieleza kuwa alilazimishwa kusaini ungamo mbele ya mlinzi wa amani bila kujua nini kilichoandikwa.

Alidai kuwa baada ya kutoka kuhojiwa kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) na Ofisa wa Makosa ya Jinai ya Mkoa (RCO), akifananishwa na picha ya gazeti la Mwananchi la Septemba 3, 2012 alipokana siyo yeye, alipelekwa kwenda kufanya ungamo kwa mlinzi wa amani, Frola Mhelela ambaye alikuwa shahidi namba tatu.

Alidai wakati anakwenda kwa mlinzi wa amani alisindikizwa na Staff Sajent Erick, ambaye alikuwa ameshika bahasha na kumkabidhi kwa mlinzi huyo.

Mtuhumiwa huyo alidai mlinzi huyo alitoa karatasi na kuisoma kisha baadaye alimuambia aisaini, naye bila kuhoji alisaini ile karatasi kwa sababu ilitoka kwa kiongozi wake ambaye ni RCO, Nyegesa Wankyo.

Katika kesi hiyo wakili wa utetezi, Rwezaura Kaijage aliiomba Mahakama kwamba mawakili wa upande wa Jamhuri wataleta majumuisho ya mwisho leo.

Hata hivyo, upande wa jamhuri ambao uliongozwa na wakili Sunday Hyera, ulisema hawana pingamizi lolote juu ya upande wa utetezi baada ya kukaa na kukubalina kwa pande zote mbili saa nane mchana watawasilisha majumuisho hayo.

Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, Dk Paulo Kihwelo alisema Mahakama imekubali ombi la wakili wa utetezi kuleta majumuisho, huku Juni 27 wakisikiliza maoni ya wazee wa baraza kwa ajili ya kupanga hukumu.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mtuhumiwa kesi ya Mwangosi akana Ungamo Lake Mahakamani
Mtuhumiwa kesi ya Mwangosi akana Ungamo Lake Mahakamani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirAfZ3niHGOQew4W2xW9DMbBDG4TrlHaeMGscYIhFW2VeZfK1SrRbbIqqDE5pQ5QL-qCksr4Zv99tor2U1hqUj1KZsyB8gJkEuqWRmKQMJ_nUzg9uv83hH3NLuUEPj6IFx0vxRNf3KEhI/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirAfZ3niHGOQew4W2xW9DMbBDG4TrlHaeMGscYIhFW2VeZfK1SrRbbIqqDE5pQ5QL-qCksr4Zv99tor2U1hqUj1KZsyB8gJkEuqWRmKQMJ_nUzg9uv83hH3NLuUEPj6IFx0vxRNf3KEhI/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/06/mtuhumiwa-kesi-ya-mwangosi-akana-ungamo.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/06/mtuhumiwa-kesi-ya-mwangosi-akana-ungamo.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy