http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Polisi Arusha yaua jambazi sugu katika Mapambano Makali ya risasi

Polisi Mkoa wa Arusha wamemuua kwa kumpiga risasi jambazi sugu aliyekuwa akisakwa kwa muda mrefu kuhusiana na matukio ya uporaji wa kutumia ...



Polisi Mkoa wa Arusha wamemuua kwa kumpiga risasi jambazi sugu aliyekuwa akisakwa kwa muda mrefu kuhusiana na matukio ya uporaji wa kutumia silaha wakati akijiandaa kufanya tukio la uporaji

Akizungumza na waandishi wa habari mapema Leo,Juni 5 ofisini kwake ,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'anzi alisema mtu huyo ambaye anadaiwa kuwa ni jambazi sugu alitambulika kwa jina moja la Riziki mwenye umri wa miaka kati ya (20 na 25) aliuawa katika mapambano ya risasi na polisi

Amesema jambazi huyo aliuliwa majira ya saa 12:00 jioni katika eneo la stendi ya mabasi madogo ya Kilombero baada ya Polisi kupata taarifa za kiintelijensia kuhusu uwepo wa jambazi huyo akijiandaa kwenda kufanya tukio na e kwenye moja ya kituo cha kuuzia mafuta kilichopo Jijini hapa.

Alisema baada ya polisi kupokea taraifa hiyo askari walikwenda eneo la tukio kwa lengo la kumkamata na mara baada ya kuwaona askari jambazi huyo alitoa silaha yake aina ya bastola aliyeificha kiunoni na kuanza kurusha risasi kwa nia ya kuwalenga askari waliokuwa wanataka kumkamata .

Aliongeza kuwa risasi moja ilimjeruhi mpita njia aitwaye Halima Salim(20) Mkazi wa Arusha kwenye mguu wake wa kulia na anaendelea na matibabu hospitali ya Mount Meru.

Alisema baada ya jambazi huyo kumjeruhi mpita njia huyo askari

walijibu mapigo kwa kupiga risasi moja ambayo ilimjeruhi juu ya tumbo

na kufariki dunia wakati akipelekwa hospitali ya Mount meru na

kusongeza kuwa marehemu alikutwa akiwa na silaha aina Chinese

iliyofutwa namba ikiwa na risasi tatu kwenye magazine na kwenye eneo

kulikutwa maganda mawili ya risasi.

Wakati huo huo, Mnamo Juni 4 mwaka huu saa 1:00 jioni katika eneo la

Ngaresero kata ya Usa River mtu mmoja wa kiume ambaye hakufahamika

jina anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 hadi 30 alikutwa amekufa

pembezoni mwa barabara huku mwili wake ukiwa na jeraha kichwani

lililotokana na kuchomwa na kitu chenye ncha kali.


Kamnada Ng'anzi alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika na

polisi wanaendelea na upelelezi huku mwili wake ukiwa umehifadhiwa katika hospital ya Mkoa Mount Meru

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Polisi Arusha yaua jambazi sugu katika Mapambano Makali ya risasi
Polisi Arusha yaua jambazi sugu katika Mapambano Makali ya risasi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0ioWC45wzD7CTOPQwmglmwsOWAVP9aRAdfKZo3e2yCB0m28_ypDNShTiyIw7lKzm3VaA-hsfip80YUcv2V_EQTbLs1FyLhVyRl1z5PR53xQKIH_v1g8qDzzHs1fL1YGCWIFEBfwneunrG/s640/IMG_20180605_112425.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0ioWC45wzD7CTOPQwmglmwsOWAVP9aRAdfKZo3e2yCB0m28_ypDNShTiyIw7lKzm3VaA-hsfip80YUcv2V_EQTbLs1FyLhVyRl1z5PR53xQKIH_v1g8qDzzHs1fL1YGCWIFEBfwneunrG/s72-c/IMG_20180605_112425.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/polisi-arusha-yaua-jambazi-sugu-katika.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/polisi-arusha-yaua-jambazi-sugu-katika.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy