http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Agizo wa Rais Magufuli uwanja wa ndege Dar laanza kutekelezwa


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Shughuli za ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam (Terminal 3) jana tarehe 09 Febr...

Mamilioni yapotea katika mazishi ya Mandela
Aliyesambaza picha za majengo UDSM atiwa mbaroni
Mtulia Atua Rasmi CCM na Kukabidhiwa Kadi....... Awajibu Wanaomtuhumu Kusaliti Upinzani

Shughuli za ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam (Terminal 3) jana tarehe 09 Februari, 2017 zimeendelea kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyefanya ziara ya kushtukiza jana tarehe 08 Februari, 2017.


Wafanyakazi 850 wameendelea na kazi mbalimbali za ujenzi wa uwanja huo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia za kuingia na kushuka kwenye ndege, mifumo ya ujazaji wa mafuta ya ndege, maeneo ya kuegeshea ndege, sehemu ya kuingia na kutoka jengoni, mifumo ya viyoyozi na ujenzi wa nguzo.


Pia, timu ya wataalamu wanaosimamia ujenzi huo imefanyiwa mabadiliko ambapo wataalamu wengine 9 kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wamepelekwa na kuanza kazi mara moja.


Mkandarasi ambaye ni kampuni ya BAM International ya Uholanzi, Mhandisi Mshauri ambaye ni kampuni ya ACE ya Misri na wafanyakazi walioajiriwa katika mradi huo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua alizochukua zilizowezesha shughuli za ujenzi kuendelea.


Katika ziara ya juzi, Mhe. Rais Magufuli alielezea kusikitishwa na utekelezaji wa mradi huo uliopangwa kugharimu Shilingi Bilioni 560 kiasi ambacho ni kikubwa mno ikilinganishwa na jengo linalojengwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa Mnyaa alikiri kuwepo kwa dosari na kuahidi kuchukua hatua.


Mhe. Rais Magufuli ameahidi kuwa Serikali inafanya juhudi za haraka kutoa malipo ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri yaliyosababisha kusitishwa kwa ujenzi.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Agizo wa Rais Magufuli uwanja wa ndege Dar laanza kutekelezwa
Agizo wa Rais Magufuli uwanja wa ndege Dar laanza kutekelezwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQyYNSFzxTfvo2xHGj6Twng6ocAOhHW7kjApf-nOqecQB3eeJ0bljPoxwpeFjWNfdkDmZ-Yv2rhkxKDeqK-lOo8q5MRTahlKzArmaLV4Nt9VSajLi3mVeixKnkKDWzQWF7IufdhwcZlZ1f/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQyYNSFzxTfvo2xHGj6Twng6ocAOhHW7kjApf-nOqecQB3eeJ0bljPoxwpeFjWNfdkDmZ-Yv2rhkxKDeqK-lOo8q5MRTahlKzArmaLV4Nt9VSajLi3mVeixKnkKDWzQWF7IufdhwcZlZ1f/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/agizo-wa-rais-magufuli-uwanja-wa-ndege.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/agizo-wa-rais-magufuli-uwanja-wa-ndege.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy