http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

BREAKING NEWS: JENGO LA PRIME HOUSE LAVAMIWA NA WATU WASIOJULIKANA

Dar es Salaam. Watu wanane wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wamevamia jengo la Prime House lililopo Mtaa wa Tambaza na kufanya uharibifu wa mal...




Dar es Salaam. Watu wanane wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wamevamia jengo la Prime House lililopo Mtaa wa Tambaza na kufanya uharibifu wa mali za wapangaji.

Jengo la Prime House lina ghorofa tano lipo jirani na ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wilayani Ilala.

Mwandishi wa gazeti hili ameshuhudia barabara ya kuingia eneo hilo ikifungwa kwa muda na polisi ambao walitumia magari yao kuziba njia na kuweka uzio wa utepe wa rangi ya njano.

Jengo la Prime House lina ofisi za kampuni mbalimbali, zikiwemo za mawakili, duka la dawa na sehemu ya kufanya mazoezi gym.

Mmoja wa mawakili ambao wana ofisi katika jengo hilo, ambaye hakutaka kutaja jina lake aliliambia gazeti hili kwamba watu hao walipofika walimfunga mlinzi kwa kamba na kisha kuingia ndani kwa nguvu.


"Mlinzi ameniambia baada ya kuingia walipokuwa wakifanya upekuzi walikuwa wakisikika wakisema si huku tutazame ghorofa linalofuata si hili,” wakili huyo amemkariri mlinzi.

Wakili huyo amesema, "Sasa nipo njia panda sijui walikuwa wanalenga ofisi gani, kwa vyovyote hawawezi kwenda gym kuchukua vifaa kwa sababu ni vizito nadhani kuna ofisi waliilenga hadi sasa sijajua kwa sababu sijaingia ndani tumekatazwa kuingia."

Amesema wanasubiri uchunguzi wa polisi ambao wapo katika harakati za kuingia ndani ya jengo hilo kujua uharibifu uliojitokeza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amethibitisha tukio hilo akisema limetokea kati ya saa nane na saa tisa usiku wa kuamkia leo.

"Kwa sasa siwezi kusema wahalifu hawa walilenga ofisi gani maana zipo nyingi katika jengo lile. Naomba mtupe nafasi tufanye uchunguzi kisha tutawapa taarifa," amesema Kamanda Hamduni

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : BREAKING NEWS: JENGO LA PRIME HOUSE LAVAMIWA NA WATU WASIOJULIKANA
BREAKING NEWS: JENGO LA PRIME HOUSE LAVAMIWA NA WATU WASIOJULIKANA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgxiM5JxumGuLnqLDDm-jdhKw3FLyJ9AJXPy_kFyZmocZwrnuVWQcDtoN-PD3blXqncTRl3Tk8XBM0YdtYg4YE03RM3CWGLBZugaEr5u3x0tK8dfQQtDQL8wjDjsE-6LLUltp-xSioPAGUU/s640/breaking-news.jpg1_.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgxiM5JxumGuLnqLDDm-jdhKw3FLyJ9AJXPy_kFyZmocZwrnuVWQcDtoN-PD3blXqncTRl3Tk8XBM0YdtYg4YE03RM3CWGLBZugaEr5u3x0tK8dfQQtDQL8wjDjsE-6LLUltp-xSioPAGUU/s72-c/breaking-news.jpg1_.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/breaking-news-jengo-la-prime-house.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/breaking-news-jengo-la-prime-house.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy