http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Mwalimu acharangwa mapanga kwa kumpa mimba mwanafunzi


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Mwalimu wa Shule ya Msingi Geitasamo iliyopo Kata ya Rung’abure wilayani Serengeti Mkoa wa Mara, Raphael Charles (22) amenusurika kufa ...

Maadhimisho ya siku ya makazi duniani yaendelea Jijini Dar es Salaam.
Rais MagufuliJP amteua Prof. Lawrence Mujungu Museru kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
WAZIRI MKUU AKAGUA MAENEO YA UJENZI DODOMA

Mwalimu wa Shule ya Msingi Geitasamo iliyopo Kata ya Rung’abure wilayani Serengeti Mkoa wa Mara, Raphael Charles (22) amenusurika kufa kwa kucharangwa mapanga kwa tuhuma za kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Ikorongo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Geitasamo, Marwa Meng’anyi alisema mwalimu huyo amejeruhiwa kwa kucharangwa mapanga na watu wanaodaiwa kuwa ni kaka wa mwanafunzi huyo baada ya kuchukizwa na kitendo cha dada yao (jina linahifadhiwa) kukatishwa masomo kwa kupata ujauzito.

Akizungumzia tukio la kucharangwa mapanga, Mwalimu Charles alisema mkasa huo ulimkumba akiwa njiani kwenda nyumbani akiwa ameongozana na mwalimu mwenzake aliyemtaja kwa jina la Frank Batholomeo.

 “Tukiwa njiani ghafla walijitokeza na kuanza kunihoji kwa nini nimempa mimba mdogo wao, kabla sijajibu mmoja wao alichomoa panga na kuanza kunishambulia akilenga kunikata shingo,” alidai Charles. 

Alidai katika jitihada za kujinusuru ilimbidi kutimua mbio, lakini alianguka chini na vijana hao kufanikiwa kumfikia na kuendelea kumshambulia kwa mapanga.

Mwalimu huyo aliyefungua kesi kuhusu shambulio hilo na kupewa namba ya jalada Mug/RB/2886/2016 la kujeruhi, alidai alinusurika kuuawa baada ya mmoja wa mafundi pikipiki waliokuwa eneo jirani kujitokeza kumsaidia. 

Tukio la kushambuliwa kwa mwalimu huyo limekuja huku madai dhidi yake kumpachika mimba mwanafunzi huyo yakiwa yamefikishwa mahakamani kwa shauri namba 82/2016 tangu Mei 13.

Akizungumzia kitendo chake na wanawe kumshambulia kwa mapanga mwalimu huyo, baba wa binti aliyepachikwa mimba, Chacha Masiko alidai familia imechukizwa na kesi dhidi ya mwalimu huyo kuahirishwa mara kwa mara bila wao kuelezwa sababu za msingi, huku mshtakiwa huyo akiwatambia mtaani kuwa hatafungwa.

Mwalimu aliyeshuhudia mwezake akicharangwa mapanga, Batholomeo alilaani kitendo cha wanafamilia hao kujichukulia sheria mkononi na kuomba mamlaka husika kuchukua hatua kukomesha vitendo hivyo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.

Kaimu Ofisa Elimu wa wilaya hiyo, Hawamu Tambwe alisema ameunda timu itakayoshirikiana na uongozi wa kijiji kuelimisha wananchi umuhimu wa kuzingatia sheria katika kushughulikia changamoto na matatizo yanayojitokeza kwenye jamii badala ya kuchukua sheria mkononi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ramadhani Ngh’azi hakupatikana kuzungumzia tukio hilo kutokana na simu yake kuita bila kupokewa, lakini mmoja wa maofisa wa polisi wilayani hapa aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina alisema jeshi hilo linawasaka ndugu hao ili wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mwalimu acharangwa mapanga kwa kumpa mimba mwanafunzi
Mwalimu acharangwa mapanga kwa kumpa mimba mwanafunzi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg67jCDMl3YQqqxYsO10IZkptzkL-TeV9J3oZhZo3flQ6CQpNJRaU_j1jc5ITlp1cE6yvFrR1YHqyuSzaQ6u64TeR_JeLnfXxt6A85ZO66BQ6NQcPhAax0QjMcqShH56PAob7haApvqjW0/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg67jCDMl3YQqqxYsO10IZkptzkL-TeV9J3oZhZo3flQ6CQpNJRaU_j1jc5ITlp1cE6yvFrR1YHqyuSzaQ6u64TeR_JeLnfXxt6A85ZO66BQ6NQcPhAax0QjMcqShH56PAob7haApvqjW0/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/mwalimu-acharangwa-mapanga-kwa-kumpa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/mwalimu-acharangwa-mapanga-kwa-kumpa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy