http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

TCCIA YAOMBA KUPUNGUZWA KWA TOZO

RAIS wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Peter Chisawilo ameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa ku...

RAIS wa Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Peter Chisawilo ameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuondoa tozo zisizo za lazima kwenye mamlaka za udhibiti ambazo zimekuwa kero inayowaongezea gharama za uendeshaji.

Chisawilo alitoa ombi hilo wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho mkoa wa Tanga.
Alisema ili kukiwezesha chama kuendelea kutekeleza majukumu na shughuli zake mbalimbali kwa uhuru, ni vema serikali ikawaondolea utitiri wa tozo ambazo zimekuwa zikilipwa sasa na mamlaka za udhibiti, hatua inayoongeza gharama za uendeshaji.

“Lengo la serikali la kuunda mamlaka na bodi za usimamizi ni kuweka utaratibu mzuri wa usimamizi na utendaji, lakini kwa sasa mamlaka hizo zimegeuza tozo kama chanzo chake cha mapato hali ambayo inawaongezea wafanyabiashara mzigo wa gharama”, alisema.
Akizungumzia fursa za biashara na uzalishaji, Chisawilo aliwataka wafanyabiashara pamoja na wamiliki wa viwanda kuhakikisha wanajiamini.

“Katika suala hili hakuna ubishi kwamba ninyi wafanyabiashara na wenye viwanda lazima mjiamini kwa kuihakikishia jamii pamoja na washindani wenu sokoni kwamba mnao uwezo wa kuzalisha bidhaa bora. Nawahimiza msiishie hapo tu, kaingieni mikataba mikubwa mfano katika mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta linalotarajiwa kujengwa kutoka Uganda hadi Tanga”, alisema.

Awali Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Tanga, Paul Bwoki akisoma taarifa ya utendaji, alisema wanachama hawana budi kuongeza ubunifu ili wanufaike na rasilimali za asili zilizopo mkoani hapa.

Katika mkutano huo ambao walichagua pia viongozi, Deo Ruhinda alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa TCCIA kwa mkoa ambapo nafasi ya makamu mwenyekiti upande wa kilimo ilichukuliwa na Juvent Magogo.
Oswin Hosea amekuwa makamu mwenyekiti upande wa viwanda pamoja na Daudi Mwai aliyechaguliwa kuwa mweka hazina.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : TCCIA YAOMBA KUPUNGUZWA KWA TOZO
TCCIA YAOMBA KUPUNGUZWA KWA TOZO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3fOYcFKYXpfGOn_opYedSGqdTczTEkHKDc0hFO_5ihoPSbQ4Bm-T99YNiFlCG_lR4-Y3S734TgdzmJqRO3zY4DkvOX-GNM9KggPj7oJyPv8EHR1WMrZRM81l5Ay1OKhO9P1GOpRQNndFc/s1600/peter-chisawilo_210_120.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3fOYcFKYXpfGOn_opYedSGqdTczTEkHKDc0hFO_5ihoPSbQ4Bm-T99YNiFlCG_lR4-Y3S734TgdzmJqRO3zY4DkvOX-GNM9KggPj7oJyPv8EHR1WMrZRM81l5Ay1OKhO9P1GOpRQNndFc/s72-c/peter-chisawilo_210_120.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/tccia-yaomba-kupunguzwa-kwa-tozo.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/tccia-yaomba-kupunguzwa-kwa-tozo.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy