http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

Magufuli: Polisi sharti wajirekebishe


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

Rais wa wa Tanzania Dkt John Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini pamoja na ofisi ya mwendesha mashitaka kujirekebisha katika ute...

Wafanyabiashara wa Mafuta ya Petrol na Dezel Dodoma Wapewa Siku 10
Muuguzi Amchoma Binti Sindano ya Usingizi na Kisha Kumbaka
Waumini wawili wafa maji wakibatizwa
Rais wa wa Tanzania Dkt John Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini pamoja na ofisi ya mwendesha mashitaka kujirekebisha katika utenda kazi na kujiepusha na kashfa.

Amesema taarifa zinaonesha jeshi la polisi limekuwa likihusishwa na matumizi mabaya ya fedha hali inayoongeza ukubwa wa matatizo yanayokwamisha utendaji wake wa kazi.

Akiongea alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi, Dodoma ametoa mfano wa taarifa za matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya kununulia vifaa na sare za askari.

Aidha, amezungumzia mikataba yenye mashaka inayotiwa saini kati ya polisi na wawekezaji akisema baadhi ya mambo yanayoongeza hali ngumu ya utendaji kazi kwa jeshi hilo.
“Nimesema lazima nizungumze kwa uwazi, nisiposema kwa uwazi nitajisikia vibaya nikimaliza mkutano huu, nataka muelewe na muelewe ukweli direction (njia) ninayoitaka mimi.”

Dkt. Magufuli pia amelitaka jeshi la polisi kujiepusha na kashfa ambazo zimekuwa zikisemwa dhidi yake, ikiwemo maafisa wa polisi kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kuazimisha silaha kwa wahalifu wa ujambazi.

Kuhusu Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, amesema amekuwa akisikitishwa sana na vitendo vya serikali kushindwa katika kesi nyingi mahakamani licha ya kuwa na wanasheria mahiri.
"Niwaombe mawakili na polisi wanaohusika na upelelezi mtangulize maslahi ya nchi mbele, kwa sababu kumekuwa na usemi kwa baadhi ya wapelelezi na mawakili wachache, nasema wachache, panapokuwa na kesi inayohusiana na pesa pesa, wana misemo yao wanasema dili limepatikana,” amesema.

“Na saa nyingine kesi inapopelekwa mahakamani wana-collude (wanakula njama) mawakili wa serikali na mawakili wanaomtetea mhalifu, na wanapo-collude (wanapokula njama pamoja) siku zote serikali inashindwa.”


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Magufuli: Polisi sharti wajirekebishe
Magufuli: Polisi sharti wajirekebishe
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi08p5C-mBUihtPDJyOZDHK8EzGuHEegJMFPNGYKVqSEfN2WM-T0bHhoFOyHt3mRZq2j1lgtqIccuA0RSXSGNtADMX8ABYyhGT6a0GfU1_cfxFfkpATZ3S3oLkqdwXmoow58VNW4nqFmDEv/s640/160429162102_john_magufuli_police_640x360_statehousetanzania.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi08p5C-mBUihtPDJyOZDHK8EzGuHEegJMFPNGYKVqSEfN2WM-T0bHhoFOyHt3mRZq2j1lgtqIccuA0RSXSGNtADMX8ABYyhGT6a0GfU1_cfxFfkpATZ3S3oLkqdwXmoow58VNW4nqFmDEv/s72-c/160429162102_john_magufuli_police_640x360_statehousetanzania.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/magufuli-polisi-sharti-wajirekebishe.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/magufuli-polisi-sharti-wajirekebishe.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy