http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Spika Ndugai ‘ampokonya’ mwenyekiti uongozi baada ya wapinzani kuitwa mbwa

Spika Job Ndugai leo amelazimika kumpokonya Najma Giga uongozi wa kikao cha Bunge baada ya mzozo uliosababishwa na mbunge wa CCM aliyewaf...

Spika Job Ndugai leo amelazimika kumpokonya Najma Giga uongozi wa kikao cha Bunge baada ya mzozo uliosababishwa na mbunge wa CCM aliyewafananisha wapinzani na mbwa.

Spika Ndugai alifanya kitendo hicho kisicho cha kawaida katika kikao cha 44 cha Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya mwaka 2018/19 ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Wakati akichangia, mbunge huyo wa Jang’ombe, Ali Omar alisema: “Ukiona majuha wanapongezana wakaona wamefanya la maana, kuna hawa mbwa kama tutawatoa itakuwa vizuri sana. Nasikia milio ya mbwa ukiwatoa itakuwa vizuri.”

Baada ya kauli hiyo, wabunge wawili kutoka Chadema, Joseph Selasini (Rombo) na Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini) walisimama kutaka utaratibu ufuatwe kwa mchangiaji kuomba radhi.

Hata hivyo, Giga hakuruhusu hilo na kusababisha wabunge wengine wa upinzani kupiga kelele wakimtaka mbunge huyo afute kauli hiyo.

Giga alitumia kama dakika mbili kuwazuia lakini hakuweza na kumtaka Omar aendelee kuchangia.

Hata hivyo hakuweza kuwazuia kutokana na wabunge hao wa upinzani kuendelea kupiga kelele wakisisitiza Omar ashinikizwe kufuta kauli yake.

Wakati kelele zikiendelea na utulivu bungeni ukitoweka, Spika Ndugai akaingia na kuchukua uongozi wa kikao na hivyo Giga, aliyeanza kuongoza kikao hicho tangu asubuhi, kulazimika kumuachia uongozi.

Credit: Mwananchi

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Spika Ndugai ‘ampokonya’ mwenyekiti uongozi baada ya wapinzani kuitwa mbwa
Spika Ndugai ‘ampokonya’ mwenyekiti uongozi baada ya wapinzani kuitwa mbwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg7HunApv6bn_Av4h5mZavnTapQsOTgWQnfXDGBs8Wkr5pp_xfepZGGKnJD9BoICvz8XgXTEN2KYszUbHe4p-EFsD6BjJSXcvqOHLH9vpmQYFtkoeh74-3xWzeTDtw8PC94aYfhuwIWMMn4/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg7HunApv6bn_Av4h5mZavnTapQsOTgWQnfXDGBs8Wkr5pp_xfepZGGKnJD9BoICvz8XgXTEN2KYszUbHe4p-EFsD6BjJSXcvqOHLH9vpmQYFtkoeh74-3xWzeTDtw8PC94aYfhuwIWMMn4/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/spika-ndugai-ampokonya-mwenyekiti.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/spika-ndugai-ampokonya-mwenyekiti.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy