http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Kenya inatarajia kurusha Satelaiti yake leo

Kenya inajiandaa kutimiza ndoto kubwa ya kisayansi leo Ijumaa. Chombo cha Satelaiti kilichoundwa nchini humo kitarushwa katika anga ...



Kenya inajiandaa kutimiza ndoto kubwa ya kisayansi leo Ijumaa. Chombo cha Satelaiti kilichoundwa nchini humo kitarushwa katika anga za juu hii leo kutoka nchini Japan.
Wanasayansi wa anga za juu kutoka Kenya waliokiunda chombo hicho tayari wako katika makao ya Uchunguzi wa Sayansi ya Anga za juu nchini Japan, (JAXA) ambapo chombo hicho kitarushwa kutoka huko.
Nchini Kenya kwenyewe raia wataweza kufuatilia shughuli hiyo moja kwa moja kwenye mtandao wa You Tube, na sherehe maalumu ya kushuhudia imeandaliwa katika chuo kikuu cha Nairobi.
Satelaiti hiyo ndogo ni ya thamani ya dola milioni moja - gharama inayoonekana kuwa ndogo kifedha kwa kiwango cha sayansi ya anga za juu.
Imebandikwa kamera mbili pamoja na vyombo vya kunasa na kupeperusha sauti.
Wahadhiri wa vyuo vikuu wanasema satelaiti hiyo inaweza kutoa huduma tofuati ikiwemo kukusanya taarifa zitakazosaidia katika kilimo na usalama, kutabiri hali ya hewa na hata kukabiliana na majanga.
Kenya kwa sasa inakabiliwa na janga la mafuriko ambalo limesababisha maafa makubwa.
Takriban watu mia mbili wamepoteza maisha yao, huku wengine zaidi ya laki mbili wamepoteza makaazi yao.
Huenda ufanisi katika uzinduzi wa satelaiti hii utaisaidia serikali pakubwa katika kujitayarisha kupambana na majanga ya aina hiyo.
Uzinduzi wa satelaiti hiyo leo unatokana na ushirikiano kati ya Idara ya Uhandisi katika Chuo Kikuu cha Nairobi, afisi ya masuala ya anga za juu ya Umoja wa Mataifa, na Shirika la utafiti wa anga za juu la Japan.
Kenya itaanza kushughulika kuunda satelaiti kubwa na bora zaidi iwapo uzinduzi wa leo utafanikiwa.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Kenya inatarajia kurusha Satelaiti yake leo
Kenya inatarajia kurusha Satelaiti yake leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk1QcqxTPOeHg67AHOnblbDZEtik70co0-Tq6cxyfjvKUkxYvYCB4Addx4XDYY-mFbYK7at8sx_kqCu7v03ErqHaVN1eIRKXxrGecI29eQw9-L_eKwBoJqN-sEnSUQAwCFbspXbd4qzd2H/s640/_101273865_f271f353-18e4-4383-acbe-c9d4a363eb31.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk1QcqxTPOeHg67AHOnblbDZEtik70co0-Tq6cxyfjvKUkxYvYCB4Addx4XDYY-mFbYK7at8sx_kqCu7v03ErqHaVN1eIRKXxrGecI29eQw9-L_eKwBoJqN-sEnSUQAwCFbspXbd4qzd2H/s72-c/_101273865_f271f353-18e4-4383-acbe-c9d4a363eb31.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/kenya-inatarajia-kurusha-satelaiti-yake.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/kenya-inatarajia-kurusha-satelaiti-yake.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy