http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Jimbo la Mbagala Kugawanywa

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeadhimia kuligawa Jimbo la Mbagala liliopo Jijini Dar ...

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeadhimia kuligawa Jimbo la Mbagala liliopo Jijini Dar es Salaam baada ya kuwepo kwa idadi kubwa ya wakazi wanaoishi jimboni humo na kusababisha uhaba wa upatikaji wa huduma za muhimu kutoka kwa Mbunge wao.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 11, 2018 na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Joseph Kakunda Bungeni Jijini Dodoma kwenye kikao cha 27 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu la nyongeza la Mbunge Mariam Kisangi aliyetaka kujua serikali inamkakati gani wa kuligawanya Jimbo la Mbagala ili liweze kufikika kiurahisi na hata Mbunge wao aweze kutoa kwa wananchi kwa wakati.

"Ni kweli Jimbo la Mbagala kwa idadi ya watu ni miongoni mwa majimbo yenye watu wengi zaidi hasa ya Dar es Salaam, lakini hivi karibuni tumeyagawa majimbo ya jiji hilo. 
"Kwa hiyo mimi nilikuwa nashauri kwa vigezo vile ambavyo nimevizungumza katika majibu ya msingi, ninaomba sasa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wakae na waweze kupendekeza na mwishowe wapeleke mapendekezo yao moja kwa moja katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)", amesema Kakunda.

Kwa mujibu wa Mbunge Mariam Kisangi amesema Jimbo la Mbagala mpaka hivi sasa lina jumla ya wananchi Milioni moja na laki moja jambo ambalo linapelekea utoaji wa huduma kuwa mgumu pamoja na kuharibika kwa miundombinu mara kwa mara kutokana na wingi wa watu waliopo jimboni humo.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Jimbo la Mbagala Kugawanywa
Jimbo la Mbagala Kugawanywa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiCNgqHuvghohbFIYSZV3Qnk25mZeKehDgO_N00J4QTfd3cql1RWgYLEQej4_j55lyAoaiexg5tbGkLk422JfhiwZXv2oDL3QNzn19itTcWYzb8tdIO1Vuj-8v4HbQCaxXJR4k1XYA-kP_H/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiCNgqHuvghohbFIYSZV3Qnk25mZeKehDgO_N00J4QTfd3cql1RWgYLEQej4_j55lyAoaiexg5tbGkLk422JfhiwZXv2oDL3QNzn19itTcWYzb8tdIO1Vuj-8v4HbQCaxXJR4k1XYA-kP_H/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/jimbo-la-mbagala-kugawanywa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/05/jimbo-la-mbagala-kugawanywa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy