http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Ufafanuzi Wa Tanesco Kuhusu Tozo Ukinunua Umeme Kupitia Simu

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limezungumzia tozo ya asilimia 1.1 wanayokatwa wateja baada ya kununua umeme kwa njia ya mitandao y...

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limezungumzia tozo ya asilimia 1.1 wanayokatwa wateja baada ya kununua umeme kwa njia ya mitandao ya simu na kupitia kwa mawakala wa benki.

Utaratibu huo ulianza Aprili 2 baada ya mfumo wa malipo wa Tanesco kuunganishwa na ule wa Serikali (GePG) ambao utawalazimu wateja wa huduma hiyo kulipia gharama za miamala husika, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo huduma hiyo ilikuwa ikitolewa bure.

Akizungumza jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka alisema kuwa bei ya umeme bado haijapanda iko palepale kama ilivyokuwa awali.

“Hizi taarifa za kupanda kwa gharama za umeme siyo za kweli, hatuwezi kufanya hivyo kwa sababu bei ilipitishwa na Ewura (Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji), hivyo hatuwezi kupandisha bila wao kuridhia,” alisema Dk Mwinuka.

Alisema tozo baada ya kununua umeme si kitu cha ajabu kwani watu wa mitandao hawawezi kumfanyia mtu huduma bila kuigharamia.

Meneja Masoko wa Tanesco, Mussa Chowo alisema utaratibu uliopo siyo mpya kwa kuwa kulikuwa na mkataba baina ya Serikali na mitandao ya simu kuwa na tozo kwa anayenunua kwa njia ya simu.

Alisema sehemu ambayo mteja atanunua umeme bila tozo ni ofisi za Tanesco, Benki ya NMB na CRDB, lakini kama watanunua kwa wakala wa benki watatozwa asilimia 1.1.

Alisema mteja akinunua umeme wa Sh5,000 atachajiwa Sh55 na atakayenunua umeme wa Sh10,000 atatozwa Sh110 na umeme wa Sh100,000 atatozwa Sh1,100.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Ufafanuzi Wa Tanesco Kuhusu Tozo Ukinunua Umeme Kupitia Simu
Ufafanuzi Wa Tanesco Kuhusu Tozo Ukinunua Umeme Kupitia Simu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEizZIhlkWUAUBmdnzAVL5Ry4O06KHmCQTPx0-AYzU9GqWJrAOvgqAFx4EW_hz5sEiiiCodeM7etCF0GmZMN83Sh2q3MkBJRXJjQvOiLnkIFoCqt1jey4Q_tE8wYXBac5M1lCB-OiZ3tRwRm/s1600/1.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEizZIhlkWUAUBmdnzAVL5Ry4O06KHmCQTPx0-AYzU9GqWJrAOvgqAFx4EW_hz5sEiiiCodeM7etCF0GmZMN83Sh2q3MkBJRXJjQvOiLnkIFoCqt1jey4Q_tE8wYXBac5M1lCB-OiZ3tRwRm/s72-c/1.png
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/04/ufafanuzi-wa-tanesco-kuhusu-tozo.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/04/ufafanuzi-wa-tanesco-kuhusu-tozo.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy