http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

CCM Mwanza yatangaza maandamano Aprili 26

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza, wanakusudia kufanya maandamano ya amani Aprili 26, mwaka huu, kuunga mkono na k...

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza, wanakusudia kufanya maandamano ya amani Aprili 26, mwaka huu, kuunga mkono na kupongeza kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli

Maandamano hayo yanakuja ikiwa ni jitihada za kuzima kile walichokiita uhuni unaofanywa na wapinzani wao kisiasa wa kutaka kuharibu amani kwa kuhamasisha maandamano ya kuchochea vurugu siku hiyo kupitia mitandao ya kijamii.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza, Paschal Mwangwala wakati wa kikao maalumu cha uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa kazi za Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Angelina Mabula kwa miaka miwili uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kiruma, jijini Mwanza na kuhudhuriwa na wajumbe 608 kati ya 748 kutoka kata 19 za jimbo hilo.

Mangwala alisema wana-CCM hawawezi kukaa kimya na kushangilia vitendo vinavyofanywa na wapinzani vya kutaka kuvunja amani, bali wazuie kwa kuandaa maandamano hayo yatakayoeleza kuwa chama pekee nchini ni CCM.

“Saidieni watu waone chama ni CCM peke yake na si vingine vinavyodandia ajenda ya kupiga kelele hiyo Aprili 26, na sisi tusaidiane maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli. Haiwezekani watu waongee vitu vya kipuuzi na kukaa kimya.”

“CCM Mwanza hatuwezi kuvumilia yeyote atakayevunja amani, yeyote atakayeleta chokochoko kwenye mkoa wetu atakiona cha mtema kuni. Yanayofanywa na viongozi wetu wa juu yashuke mpaka kule chini, wananchi waone, viongozi wa mitaa waunge juhudi hizi,” alisema.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ilemela, Nelson Mesha alisema kinachofanywa na vyama vya upinzani nchini ni dalili tosha kuwa vimefikia mwisho na vimekosa hoja na badala yake vinakimbilia kufanya maandamano.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : CCM Mwanza yatangaza maandamano Aprili 26
CCM Mwanza yatangaza maandamano Aprili 26
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEge_xzfP2S2r2aQd4npAuGZx1F3uE0nFe6-ZBiKyrex1Wue6fhK4IYQynjHG-70tIeCOnREeZUWf07sBSaYWu-fG8BmQTekrHdA2vu3L8PUOKIvHkYOMA2vfXhPIYWAO9jATYqOwHVHpHlJ/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEge_xzfP2S2r2aQd4npAuGZx1F3uE0nFe6-ZBiKyrex1Wue6fhK4IYQynjHG-70tIeCOnREeZUWf07sBSaYWu-fG8BmQTekrHdA2vu3L8PUOKIvHkYOMA2vfXhPIYWAO9jATYqOwHVHpHlJ/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/04/ccm-mwanza-yatangaza-maandamano-aprili.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/04/ccm-mwanza-yatangaza-maandamano-aprili.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy