http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Urusi Nayo Imejibu Mapigo.....Wanadiplomasia 60 wa Marekani Watimuliwa, Ubalozi Wafungwa

Urusi imewafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani, na kufunga ubalozi uliopo St Petersburg ikiwa ni majibu kwa kitendo cha Marekani kuwaf...

Urusi imewafukuza wanadiplomasia 60 wa Marekani, na kufunga ubalozi uliopo St Petersburg ikiwa ni majibu kwa kitendo cha Marekani kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi juu ya shutuma ya Uingereza kuhusu kuhusika kwa Urusi katika shambulio la jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Kripal na binti yake huko Uingereza.

Hatua hiyo ilitangazwa na waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov. Zaidi ya nchi ishirini zimewafukuza wanadiplomasia wa urusi nchini mwao katika kuunga mkono Uingereza.

Miongoni mwa nchi hizo ni Marekani ambapo mapema wiki hii iliwatimua wanadiplomasia 60 wa urusi kuondoka Marekani.

Katika kujibu hilo Urusi imewatimua wanadiplomasia 58 kutoka Moscow na wawili kutoka mji wa Yekaterinburg, chombo cha habari cha Interfax kiliripoti.

Lavrov alisema kuwa nchi nyingine zilizowafukuza Warusi wasubiri majibu kwa vitendo.

Ameongeza kuwa Ubalozi wa Marekani umepewa taarifa juu ya hatua hiyo kama majibu kwa Marekani kwa kuwatimua wanadiplomasia wake na kusimamisha ubalozi ulioko St. Petersburg.

Baada ya hatua hiyo msemaji wa Marekani amesema kuwa Urusi haina nia ya kuwa na uhusiano mzuri na nchi nyingine, na hivyo Marekani ina haki ya kuchukua hatua nyingine dhidi ya Urusi.

''Urusi imeamua kujitenga zaidi yenyewe, tunaangalia maamuzi ya kuchukua'' Heather Nauert aliwaambia waandishi wa habari.
 
Urusi imekataa kuhusika kwa namna yoyote na jaribio la mauaji kwa jasusi wake wa zamani. Kripal bado yupo katika hali mbaya hospitalini lakini Binti yake anaendela vizuri na ameondoka katika hali ya hatari.

Kutokana na kuhusishwa kwa Urusi na tukio hilo mapema Uingereza ilisema kuwa hawatatuma mawaziri wake pamoja na familia ya Malkia kushiriki kombe la dunia.

Itakumbukwa kuwa mwaka 1986 Rais wa Marekani Ronald Reagan aliwatimua wanadiplomasia 80 wa Urusi.

Na mwaka 2016 uongozi wa Barack Obama uliwafukuza wanadiplomasia 35 kutokana na kudukua chama cha Democratic.

Credit:BBC

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Urusi Nayo Imejibu Mapigo.....Wanadiplomasia 60 wa Marekani Watimuliwa, Ubalozi Wafungwa
Urusi Nayo Imejibu Mapigo.....Wanadiplomasia 60 wa Marekani Watimuliwa, Ubalozi Wafungwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgG8mUEq6kTzaxyRWcecRR3N3V6r7A36ya5nVbXPX8QO42zhY8dNYf2VlbVtKAhxjqb-0KGWkBQ0ZAvss8jE7nbtVQ0yCUAR6glrDYsZUPvLGh0Px7_MOT_tcBbmCEMpPZdlWvGByDxCLv0/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgG8mUEq6kTzaxyRWcecRR3N3V6r7A36ya5nVbXPX8QO42zhY8dNYf2VlbVtKAhxjqb-0KGWkBQ0ZAvss8jE7nbtVQ0yCUAR6glrDYsZUPvLGh0Px7_MOT_tcBbmCEMpPZdlWvGByDxCLv0/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/03/urusi-nayo-imejibu-mapigowanadiplomasia.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/03/urusi-nayo-imejibu-mapigowanadiplomasia.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy