http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

RPC Mkumbo Apumzishwa ICU hali yake hii hapa wengi wamiminika Mount Meru

Hali ya Maendele ya Afya ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ,Charles Mkumbo ambaye amelazwa katika hospitali ya mkoa Mount Meru baada...

Hali ya Maendele ya Afya ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ,Charles Mkumbo ambaye amelazwa katika hospitali ya mkoa Mount Meru baada ya kupata ajali jana akitokea Mkoani Singida inaendelea vizuri.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo ofisini kwake mganga mkuu wa Hospitali hiyo  ,Jackline Urio amesema kuwa wamelazimika kumpumzisha katika chumba cha wagonjwa mahututi( ICU) ili apate muda mzuri wa kupumzika na hali yake ni nzuri.

"Hospitali yetu haina vyumba binafsi vya wagonjwa ndio maana tumeamua kumpumzisha chumba cha ICU na sio kwamba yupo mahututi hali yake ni nzuri"Amesema
Aidha amesema kwamba Mkumbo alifikishwa katika hospitali hiyo jana majira ya jioni na kufanyiwa upasuaji baada ya kuumia sehemu ya Kichwa ,na kidole cha mkono wa kushoto ambacho kimevunjika.

Hata hivyo mganga mkuu amesema kuwa pamoja na afya ya majeruhi kuendelea vizuri anapaswa kutumia muda mwingi  kupumzika kutokana na majeraha  kichwani yaliyotokana na kukatwa na vyoo vya gari.

Watu mbalimbali mashuhuri wamekuwa wakimiminika katika hospitali hiyo kwà lengo la kumjulia hali ingawa uongozi wa hospitali hiyo umezuia kumwona 

Naye kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Arusha ,Yusufu Ilembo  ,amesema kuwa mkumbo alipata ajali jana majira ya saa 8 mchana katika eneo la Mdorii ,wilayani Babati mara baada ya gari alilokuwa akitumia lenye namba PT 2040 kupasuka tairi la nyuma na kupinduka.

Mkumbo alikuwa akitumia gari la polisi aina ya Landcruser V8,lililokuwa likiendeshwa na dereva aliyetambuliwa kwa jina la staff sajenti Silvanus ambaye naye alipata majeraha ya mguu huku mlinzi wa kamanda huyo akitoka mzima wa Afya.
Aliongeza kuwa huenda akaruhusiwa siku za usoni kuanzia kesho kutokana na halinyake kutengamaa.
Mwisho

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : RPC Mkumbo Apumzishwa ICU hali yake hii hapa wengi wamiminika Mount Meru
RPC Mkumbo Apumzishwa ICU hali yake hii hapa wengi wamiminika Mount Meru
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgofwjIJQ-2PWL0fwRISM-6jxsbvOnBmV0vxA_MYAdNjeaA4FSwyYCzylbDdakbdKJvX08RzV5U4CxgDl7_lq1A_CZsSJOywLKDOAZRmVnu_Vk1F_s0oeZx-Bog3VFIVx0ekRGX6-Wmtv3_/s640/IMG-20180226-WA0032.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgofwjIJQ-2PWL0fwRISM-6jxsbvOnBmV0vxA_MYAdNjeaA4FSwyYCzylbDdakbdKJvX08RzV5U4CxgDl7_lq1A_CZsSJOywLKDOAZRmVnu_Vk1F_s0oeZx-Bog3VFIVx0ekRGX6-Wmtv3_/s72-c/IMG-20180226-WA0032.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/rpc-mkumbo-apumzishwa-icu-hali-yake-hii.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/rpc-mkumbo-apumzishwa-icu-hali-yake-hii.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy