http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

RAIS WA WANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Kifo cha Mwanafunzi wa Chuo kikuu nchini Kenya kimezuaa shutuma mpya za mauaji yanayodaiwa kutekelezwa na maafisa wa polisi nchini humo...

Kifo cha Mwanafunzi wa Chuo kikuu nchini Kenya kimezuaa shutuma mpya za mauaji yanayodaiwa kutekelezwa na maafisa wa polisi nchini humo.
Ripoti zinasema Evans Njoroge, mwanafunzi ambaye alikua kiongozi Chuo kikuu cha Meru nchini humo, aliuawa kwa kupigwa risasi na anayedaiwa kuwa polisi.
Mwandishi wa BBC, Ferdinand Omondi anasema pichaza mwili wa kijana huyo, damu yake ikionekana imetapakaa kote, zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii huku raia wa Kenya wakighadhabishwa na kile walichodai kuwa mauaji yanayotekelezwa na polisi.
Evans alipigwa risasi Jumanne wakati wa maandamano ya wanafunzi waliokuwa wakilalamikia ongezeko la ada dhidi ya chuo cha Meru.
Vyombo vya habari nchini Kenya vimemnukuu shuhuda mmoja akisema polisi walimkimbiza Evans wakamfikia kisha mmoja wao akampiga risasi na kuondoka.
Mkuu wa polisi Jenerali Joseph Boinnet ameamuru kufanyika uchunguzi kuhusu kifo hicho baada ya kuwepo kwa wanasiasa na makundi ya wanaharakati waliokuwa wakitaka mauaji yanayodaiwa kutekelezwa na polisi kukoma mara moja.
Shirika huru la kiraia linalofuatilia shughuli za polisi (IPOA) limesema limewatuma maafisa wake kuchunguza tukio hilo.
Mwanafunzi huyo aliuawa katika eneo la Nchiru, eneo la Tigania West katika jimbo la Meru ambalo linapatikana katika eneo la Mlima Kenya.
IPOA wamesema maafisa wa uchunguzi wametukwa kwa lengo la: "kuchunguza kuhusu yaliyotokea wakati wa mauaji hayo na iwapo kuna mtu anayefaa kulaumiwa, na kuhakikisha afisa yeyote wa polisi atakayepatikana na hatia anawajibishwa kisheria."
Wakenya mtandaoni wamekuwa wakishutumu mauaji hayo.
Shutuma hizi mpya zimekuja siku kadhaa baada ya shirika linalotetea haki za binadamu la Human Rights Watch kuwasilisha ushahidi mpya kuwa polisi nchini Kenya waliua watu takriban 23 wakati wa kipindi cha marudio ya uchaguzi nchini humo mwaka jana.
Kwa mujibu wa ripoti,uchunguzi umebaini kuwa wengi wa waathirika walifyatuliwa risasi na silaha za nguvu.
Polisi wameendelea kukana shutuma hizo.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : RAIS WA WANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI
RAIS WA WANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjNOedOzO14hG4uiizzhIBAwoupkaKq7VDKiItZ65hGMzsbhIUSEFxW04MyuFUmY4hY0c2ebuZyxCGxLcykS_CG2quPxGmF6O_MHn_K69dcmJgXYYhf-HVpDIWFmmeSxHE1sGi3wNocNequ/s640/_100214170_742c4f55-f124-47c6-ba11-29790fe35ead.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjNOedOzO14hG4uiizzhIBAwoupkaKq7VDKiItZ65hGMzsbhIUSEFxW04MyuFUmY4hY0c2ebuZyxCGxLcykS_CG2quPxGmF6O_MHn_K69dcmJgXYYhf-HVpDIWFmmeSxHE1sGi3wNocNequ/s72-c/_100214170_742c4f55-f124-47c6-ba11-29790fe35ead.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/rais-wa-wanafunzi-auawa-kwa-kupigwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/rais-wa-wanafunzi-auawa-kwa-kupigwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy