http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mchungaji Akiponza Kituo cha Redio Chafungiwa na Kutozwa Faini ya Milioni 2

Serikali ya Rwanda kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Mawasiliano nchini humo (RURA), imekifungia kituo cha redio ya kidini cha  ...

Serikali ya Rwanda kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Mawasiliano nchini humo (RURA), imekifungia kituo cha redio ya kidini cha  Amazing Grace 105.1 FM kurusha matangazo kwa kipindi cha mwezi mmoja pamoja na kulipa faini ya faranga milioni 2 sawa na Tsh milioni 6, baada ya redio hiyo kurusha matangazo yaliyowadhihaki wanawake kwa kuwataja kuwa ndiyo chanzo cha matatizo duniani.

Mamlaka hiyo imeeleza kuwa mnamo Tarehe 29 Januari 2018 Mchungaji wa Kanisa la Kisabato, Niyibikora Nicholas akitangaza injili kupitia kituo hicho cha redio alisikika hewani akisema wanawake ni moto wa kuotea mbali kwani ndo chanzo cha maovu na migogoro isiyoisha duniani.
Mchungaji huyo akiwa LIVE hewani aliendelea kusema kuwa hata Mungu hawapendi wanawake, kwani mwanamke hajawahi kuwa mtu mwema tangu enzi za bustani ya edeni ambapo alikula tunda alilokuwa ameambiwa asile na kumshawishi na mumewe kufanya dhambi.

Mamlaka hiyo ilichambua mahubiri yake yote ambapo imeeleza kuwa maudhui yote yalitoa mifano lukuki ya kwenye biblia inayowaelezea wanawake kuwa ni watu wabaya huku mchungaji huyo akiwataka wanaume wasiwaamini wanawake kwani wanawake ni watu wabaya.

Mhubiri huyo alizua mjadala mzito kwenye mitandao ya kijamii nchini Rwanda na kuwakasirisha wanawake ambapo Mwavuli wa Utetezi wa Haki za Wanawake Rwanda (Profemmes Twese Hamwe) na Jukwaa la Waandishi wa Habari wa Kike Rwanda (ARFEM) walipaza sauti zao kutaka achukuliwe hatua kwa tuhuma za uchochezi wenye misingi ya kijinsia na kulenga kusababisha mtafaruku kwenye jamii.

Tayari Ofisi ya Mwendeshaji Mkuu wa Mashtaka imeliagiza jeshi la polisi kitengo cha upelelezi wa makosa ya jinai kuanza upelelezi juu ya madai yanayomkabili Mchungaji huyo.
Chanzo:The New Times

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mchungaji Akiponza Kituo cha Redio Chafungiwa na Kutozwa Faini ya Milioni 2
Mchungaji Akiponza Kituo cha Redio Chafungiwa na Kutozwa Faini ya Milioni 2
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6RDPq18OONy1mywhze4I6Zckl2F9PkJSopFRD7nrV2ZoHCuwzqB5bloR0dwG_ykmfqoe3yh9vYzFkQ9zLpdJ-zTR7L4WZj18jxGklHOVXWrOCuoAH-QSuCZihDzsmDtvZGg4Sjc7BDfg/s640/amazinggracefm.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6RDPq18OONy1mywhze4I6Zckl2F9PkJSopFRD7nrV2ZoHCuwzqB5bloR0dwG_ykmfqoe3yh9vYzFkQ9zLpdJ-zTR7L4WZj18jxGklHOVXWrOCuoAH-QSuCZihDzsmDtvZGg4Sjc7BDfg/s72-c/amazinggracefm.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/mchungaji-akiponza-kituo-cha-redio.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/02/mchungaji-akiponza-kituo-cha-redio.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy