http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Umri wa kustaafu kazini waongezwa

Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma. Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha muswaada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalim...

Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha muswaada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298  (The Public Service Act) itakayowezesha muda wa kustaafu kwa  Wahadhiri waandamizi, Maprofesa na Madaktari Bingwa kuwa miaka 60 kwa hiari na lazima miaka 65.
Akizungumza wakati akiwasilisha muswaada huo  Mwanasheria  Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju amesema kuwa marekebisho katika jedwali yanapendekeza kuongezwa kwa kifungu kipya cha 25A ambacho kinaainisha kuhusu umri wa kustaafu ambapo kwa sasa sheria ilivyo  haina masharti hayo isipokuwa umri wa kustaafu umetajwa katika sheria zinazoanzisha mifuko ya hifadhi za jamii.
Aliongeza kuwa, uzoefu umeonyesha kuwamba Maprofesa na Wahadhiri waandamizi wa vyuo  Vikuu  vya Umma pamoja na madaktari Bingwa wa Binadamu wa Hospitali za Umma wamekuwa wakihitajika kuendelea kutoa huduma, utaalamu na uzoefu wao licha yakufikisha umri wa miaka 60 kwa sasa ya kustaafu na hivyo kulazimika kuajiriwa na Serikali kwa mikataba.
Hatua yakuwaajiri wataalamu hao kwa mikataba baada ya kustaafu imetajwa kuongeza gharama kubwa kwa Serikali ambapo muswaada ulipitishwa  unawezesha Serikali kuokoa Kiwango kikubwa cha fedha zilizokuwa zikitumika katika kuwalipa wataalamu wao mara baada ya kustaafu ili waweze kufanya kazi kwa mikataba.
Kwa upande wake Waziri  wa Elimu Sayansi na Teknplojia mhe. Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa anaunga mkono hoja  yakuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 60 kwa lazima hadi 65 na kutoka miaka 55 kwa hiari hadi miaka 60.
Aliongeza kuwa Serikali inayo mikakati ya makusudi yakuwaendeleza wataalamu wa kada zenye uhaba  wataalamu wabobezi ili kuziba pengo  lililopo.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wake wa 10 kikao cha 1 limepitisha muswaada wa marekebisho ya sheria mbalimbali nne ambazo ni Sheria ya Ufilisi, sura ya 25, Sheria ya Bajeti, sura ya 439, Sheria ya Ardhi, sura ya 113 na Sheria ya Utumishi wa Umma, sura ya 238.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Umri wa kustaafu kazini waongezwa
Umri wa kustaafu kazini waongezwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIrARS-Pq0MV1iBzjjFrBcWCXiZB9MSEqPSukOqXPijFtYaNefdU8SsRghGZA0eNnqvkazWPiB2eJJ5yyeZg6ZitPnwrWws32HZUrs8H_T2TVaKhMi_E3ciqIaz8gtjBWMc-U44uIqgkIZ/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIrARS-Pq0MV1iBzjjFrBcWCXiZB9MSEqPSukOqXPijFtYaNefdU8SsRghGZA0eNnqvkazWPiB2eJJ5yyeZg6ZitPnwrWws32HZUrs8H_T2TVaKhMi_E3ciqIaz8gtjBWMc-U44uIqgkIZ/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/umri-wa-kustaafu-kazini-waongezwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/umri-wa-kustaafu-kazini-waongezwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy