http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mgombea Ubunge CHADEMA Jimbo la Kinondoni Atoa Neno Zito Akirudisha Fomu Leo

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalimu amefanikiwa kurudisha fomu ya kugombea Ubunge ji...

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalimu amefanikiwa kurudisha fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Kinondoni huku akiwataka wanachama wa chama hicho kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha muda mfupi.

Mhe. Salum ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari vilivyoweza kujitokeza katika ofisi za Tume ya Uchaguzi Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo alasiri(Jumamosi).

"Nimefarijika kwamba fomu imepokelewa na haina mapungufu yeyote yale, kwa hiyo hatuna shaka lolote katika fomu yetu kwa maana tumeikagua na kuuliza maswali katika kipengele jinsi tulivyojaza na wakatujibu tupo sahihi. Imani yangu ni kwamba hawajaona kosa ambalo wanaweza kulikalia kimya walisubiri ili lilete matatizo baadae", alisema Mhe. Salum Mwalimu.

Aidha, Mhe. Salum aliendelea kufafanua baadhi ya mambo kwa kusema hatoweza kutangaza siku ya kuanza kampeni rasmi mpaka itakapofika alasiri ya kesho (Jumapili) kwa maana muda huu wa katikati ameuacha ili kama kutakuwa na watu waweze kuweka mapingamizi yao.

"Kwa hiyo baada ya muda huo kupita siku ya kesho bila ya shaka nitakuwa mgombea rasmi wa jimbo la Kinondoni ambaye nisiyekuwa na doa kwa ajili ya mapambano hayo", alisistiza Mhe. Salum Mwalimu.

Pamoja na hayo, Mhe. Salum aliendelea kwa kusema "kikubwa labda niwaambie hatukuja ku-beep wala hatu-beep kamwe haitakuja kutokea ku-beep katika jimbo la Kinondoni. Tunamaanisha na tunaamini kabisa kama nidhamu ya siasa waliyoikataa, hapa watairudisha na wasipoikubali kuirudisha Kinondoni maana yake ustaarabu katika siasa tunaamini utakuwa umekwishamalizika. Hatutokuwa wa kulia, safarii hii ikibidi tutawasababisha wale waliosababisha sisi tunalialia wao ndio walie".

Kwa upande mwingine Mhe. Salum Mwalimu amesema amedhamilia na amejitoa kusimamia haki ya wananchi wa Jimbo la Kinondoni na kuahidi hatoweza kuyumba katika hilo.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mgombea Ubunge CHADEMA Jimbo la Kinondoni Atoa Neno Zito Akirudisha Fomu Leo
Mgombea Ubunge CHADEMA Jimbo la Kinondoni Atoa Neno Zito Akirudisha Fomu Leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg8x1fd0xJqRtnpWkZxc0rRKx5YNiFUjeb2uUdMdzhMGZjGaTsL3jGOi4N3zVkwJUCam5pv3K3XmOGq6I01xd4Bvv9gYHnbuoGs_XamH2ZGnOvTTTsC_EmXX2aIcPM3dqiyqGImO_dVJB5l/s1600/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg8x1fd0xJqRtnpWkZxc0rRKx5YNiFUjeb2uUdMdzhMGZjGaTsL3jGOi4N3zVkwJUCam5pv3K3XmOGq6I01xd4Bvv9gYHnbuoGs_XamH2ZGnOvTTTsC_EmXX2aIcPM3dqiyqGImO_dVJB5l/s72-c/1.JPG
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/mgombea-ubunge-chadema-jimbo-la.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/01/mgombea-ubunge-chadema-jimbo-la.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy