http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Kama Ulishiriki Kusambaza Ujumbe Huu Basi Imekula Kwako!

Hatimaye, uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) umekanusha juu ya taarifa ambazo zilikuwa zinasambaa zikiwahusu vigogo wa shirik...

Hatimaye, uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) umekanusha juu ya taarifa ambazo zilikuwa zinasambaa zikiwahusu vigogo wa shirikisho hilo wakiongozwa na rais wao, Wallace Karia kujilipa posho ya kiwango cha juu.
 
Hivi karibuni kulisambaa taarifa mitandaoni juu ya vigogo hao wa TFF kujilipa fedha nyingi.

Kumbuka viongozi wa kuchaguliwa TFF hawapati mishahara, badala yake wanalipwa posho, sasa ilielezwa kwamba Karia analipwa Sh milioni sita, makamu wake Sh milioni tano huku wajumbe wa Kamati ya Utendaji wakilipwa milioni moja kwa kila mwezi.
 
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao, amesema suala hilo halina ukweli na kudai kuwa Karia alikataa kulipwa na kusisitiza posho yake ipelekwe katika masuala mingine ya kimpira kwa kuwa yeye ni muajiriwa serikalini na analipwa mshahara huko.
 
“Hizo taarifa hazina ukweli wowote kwa sababu viongozi wa hapa hakuna ambaye anachukua kiasi hicho cha fedha.
“Hata kwenye suala la wajumbe, nao hakuna ambaye anapokea shilingi milioni moja kwa mwezi kama inavyosemekana badala yake tunatoa shilingi milioni moja na nusu kwa miezi mitatu tena kwa yule ambaye anachakarika na tunaona juhudi zake kwa kupitia ripoti ambazo anawasilisha kwenye vikao.
 
“Lakini kwa sababu jambo hilo limechafua sura ya taasisi yetu tuna mpango wa kuwafungulia kesi ya makosa ya kimtandao wale wote ambao wamehusika kwenye suala hilo na tayari tuna majina 10 ya watu ambao tutaanza nao,” alisema Kidau.

Pamoja na TFF kuamua kulitolea ufafanuzi suala hilo, bado inaonekana haukuwa mjadala mpana hasa nje ya mitandao na huenda waliamua kuwahi mapema ili kumaliza mjadala.
 
WARAKA WA TUHUMA UNAZOSAMBAZWA NI HUU;
“KAMATI TENDAJI YA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF) KUTUMIA MILIONI 438 KWA MWAKA  KUJILIPA POSHO.
Tarehe 28/10/2017 Kamati ya Utendaji ya TFF, ilifanya Kikao katika Hoteli ya SEA SCAPE Kunduchi Beach jijiji Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine ilipitisha azimio la Wajumbe wa Kamati hiyo kuanza kulipwa posho  ya kila mwezi kwa mchanganuo ufuatao: 
 
1. Rais wa  TFF  Tsh.Mil.6 kwa mwezi  sawa na Mil.72 kwa Mwaka.
2. Makamu wa Rais wa TFF, Tsh. mil. 5  kwa mwezi sawa na Mil.60 kwa mwaka.
3. Wajumbe 20 wa Kamati ya Utendaji kila mmoja Tsh. Mil. 1 kwa mwezi sawa na mil.12 kwa mwaka ,  kwa wajumbe 20 ni Tsh.  Mil. 240 kwa mwaka.
 
NB: Posho hizi ni mpya na hazijawahi kuwepo katika shirikisho hilo katika uongozi uliopita.  
 
Aidha Posho za kila kikao zimepanda kutoka Tsh. 300, 000/=  uongozi uliopita hadi laki tano (500,000/) uongozi wa sasa kwa kila mjumbe,  kwa mwaka kuna vikao vya kawaida visivyopungua sita,  kwa Wajumbe wote 22 kwa mwaka itakuwa mil.66. 
 
Kwa  mchanganuo huo, Gharama za Posho tu kwa mwaka kwa Wajumbe wa  Kamati ya Utendaji tu ni milioni mia nne thelathini na nane (mil.438). Bado posho za vikao vya dharura, posho za watumishi wengine n.k
 
Moja ya changamoto za maendeleo ya Mpira wa Miguu Tanzania ni Ukosefu wa fedha.  Timu zetu za taifa zinashindwa kukaa kambini,  Waamuzi wanakosa Mafunzo, viwanja vya michezo vinashindwa kuboreshwa, vilabu vya michezo havisaidiwi na mambo mengine chungu nzima hayafanyiki sababu ya ukosefu wa fedha, leo hii EXCOM  inakwenda kujifungia Sea ESCAPE na kuidhinisha  mil. 438 kwa ajili kujilipa posho!  
Kwa mwendo huu tusitegemee maendeleo katika soka Tanzania. Rais wa TFF,  WALES KARIA na Makamu wake, MICHAEL WAMBURA wanapaswa kujitathmini upya,”.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Kama Ulishiriki Kusambaza Ujumbe Huu Basi Imekula Kwako!
Kama Ulishiriki Kusambaza Ujumbe Huu Basi Imekula Kwako!
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0QjOvWBmZcZA-HI5Y70_yKh86ZJ3uhwf5UjmRx4OX06UkzRxG31_hg7CjMTSG0pQaGwvWAg56JD1zhxDdXlCStVq_DpzKYy_3YXfT_bNOxGHv_2NRligDiURyc6tgmlBpQSpsRD87Bnwr/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0QjOvWBmZcZA-HI5Y70_yKh86ZJ3uhwf5UjmRx4OX06UkzRxG31_hg7CjMTSG0pQaGwvWAg56JD1zhxDdXlCStVq_DpzKYy_3YXfT_bNOxGHv_2NRligDiURyc6tgmlBpQSpsRD87Bnwr/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/11/kama-ulishiriki-kusambaza-ujumbe-huu.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/11/kama-ulishiriki-kusambaza-ujumbe-huu.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy