http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Lema amjibu IGP kuhusu dereva wa Lissu

Mbunge  Godbless Lema amefunguka na kusema maneno aliyosema IGP Sirro jana kuhusu dereva wa Lissu ni dhihaka kubwa kwa...


Mbunge  Godbless Lema amefunguka na kusema maneno aliyosema IGP Sirro jana kuhusu dereva wa Lissu ni dhihaka kubwa kwa ndugu wa Lissu, wanachama wa CHADEMA na hata viongozi wa chama hicho na kusema hakustahili kusema maneno yale kama IGP.  

Lema amesema hayo baada ya IGP Sirro kusikika katika baadhi ya vyombo vya habari akiwa Mtwara akisema kuwa dereva wa Tundu Lissu ndiyo anachelesha uchunguzi wa sakati hilo hivyo aliomba arudi ili kulisaidia jeshi la polisi kutoa taarifa ili kufanikisha upelelezi wa sakata la kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.
"Kamanda Sirro amesikika akiwa Mtwara akisema jeshi la polisi linamuhitaji dereva wa Tundu Lissu kwa ajili ya kukamilisha mahojiano ya upelelezi na kwamba tunasema au CHADEMA inasema anaumwa wakati dereva akionekana akipiga picha anang'ara kabisa, hii ni lugha ya mzaa na lugha ya kadhia hasa kwa familia na sisi wanachama wenzake na Tundu Lissu na hasa kwa dereva mwenyewe ambaye alishuhudia na kusikia milio ya risasi zaidi ya 30 na leo si tu kwamba anatatizo la kisaikolojia kwake binafsi lakini amuona boss wake, kaka yake na mzee wake wa siku nyingi akiwa kitandani akisubiri kudra za Mwenyezi Mungu kuweza kuishi hivyo hii ni kauli ya mdhaa ni kauli ambayo haikupaswa kutolewa na IGP" alisema Lema 
Mbali na hilo Lema amelitaka jeshi la polisi kukamilisha kwanza upelelezi wa matukio ya kupotea kwa Msaidizi wa Mbowe, Ben Sanane kifo Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo ambao wao hawakuwa hata na madereva lakini mpaka sasa jeshi la polisi limeshindwa kutoa ripoti juu ya matukio hayo.
"Leo wanaposema dereva wa Lissu anachelewesha upelelezi kukamilika siyo kweli kwa sababu Ben Sanane hakuwa na dereva na mpaka leo hatujawahi kuona mchakato wa suala lake kukamilika, Mawazo pia hakuwa na dereva lakini mpaka leo tunaushuhuda kwamba waliopo jela walishawahi kugoma barabarani na kusema wao hawakuwa wahusika wa tukio lile, wapo watu wengi wa CHADEMA wameuwawa lakini hawakuwa na madereva kama wameshindwa kukamilisha kwanza upelelezi huo ni mtake kwanza Sirro akamilishe kwa haraka suala la Ben Sanane ambalo kimsingi wamekataa kufanya utafiti wake, tunajua serikali haiwezi kufanya uchunguzi wa tukio la Lissu kwa sababu wanajua nini kimefanyika" alisema Lema 

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Lema amjibu IGP kuhusu dereva wa Lissu
Lema amjibu IGP kuhusu dereva wa Lissu
http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2017/10/05/Lema%20.jpg?itok=d25dv6FC×tamp=1507200094
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/10/lema-amjibu-igp-kuhusu-dereva-wa-lissu.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/10/lema-amjibu-igp-kuhusu-dereva-wa-lissu.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy