http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Wabunge CHADEMA kumuamshia dude Magufuli kwa hili

Baada ya Rais Magufuli kuhutubia Arusha katika shughuli za kuwatunukia Kamisheni Maafisa ya Jeshi la Wananchi JWTZ na ...


Baada ya Rais Magufuli kuhutubia Arusha katika shughuli za kuwatunukia Kamisheni Maafisa ya Jeshi la Wananchi JWTZ na kisha kuwapa nafasi Madiwani kumi waliohama Chadema kwa madai ya kumuunga Rais mkono Wabunge wa Arusha wametaka kukutana na Rais 
ili wamuoneyeshe rushwa ilivyotumika na watumishi wake.

Kupitia ujumbe wa Video uliowekwa na viongozi hao mtandaoni, Godbless Lema wa Arusha Mjini  pamoja na Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki wamemtaka Rais Magufuli kuwapatia nafasi za kuweza kumthibitishia jinsi viongozi wake walivyoweza kutumia rushwa na kuwashawishi madiwani hao wa Chadema kuachia ngazi na kumhakikishia kuwa ushahidi wote wanao hivyo wao wapo tayari kumuonyesha hata mbele ya vyombo vya usalama.

Mh. Lema amesema kuwa wao kama Chadema hawana shida kwa viongozi hao kuondoka ndani ya chama chao na hata kama wataondoka wote, lakini wanachosikitika ni jinsi viongozi hao walivyofanya vitendo vya aibu na vya kumdhalilisha Mh. Rais kwa kutumia rushwa.
"Tuna taarifa tulizipata kwamba leo madiwani wawili wa Arusha mjini wangeondoka na kujiunga na CCM lakini kwetu siyo shida, Mh. Rais anapaswa kufahamu kwamba hakuna chochote kitakachofanyika kwenye ofisi za Mkuu wa mkoa, Mkuu wa Wilaya au Mkurugenzi ndani ya Arusha na sisi tusikipate. Sasa Mh. Rais. Mimi nataka umuite Nasarri, RPC, IGP na hata Takukuru tukupatie ushahidi. Mimim sitaweza kuja maana najua sipendwi sana.

Ameongeza kwamba "Tulikuwa tunasubiri tukio la leo, wewe ni Rais mcha Mungu na Kiongozi unayepinga Rushwa, hawa watu wanaosema wamejiunga na Chama chao utajua wamejiunga kwa sababu ya kukuunga mkono au wameunga rushwa na fedha mkono.  Hawa watu walioandaa hafla Mh. Rais wamekutia aibu sana na tutoe angalizo kwamba ushahidi huu haupo nyumbani kwetu msije kutufata upo hewani na mkituletea shida tutawaambia vijana wabonyeze Button ili usambae au pia usikutana na Nassari tutauachia.

Kwa Upande wa Mbunge Joshua Nassari amesema kesho watafanya mkutano na wanahabari na kuelezea rushwa ilivyotumika na viongozi kumdanganya Rais wa nchi na kusisitiza ushahidi wao hauna mashaka.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Wabunge CHADEMA kumuamshia dude Magufuli kwa hili
Wabunge CHADEMA kumuamshia dude Magufuli kwa hili
http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2017/09/23/GodBless%20Lema.jpg?itok=ExqqV1Gw×tamp=1506187121
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/wabunge-chadema-kumuamshia-dude.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/09/wabunge-chadema-kumuamshia-dude.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy