http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Wana Chadema 51 mbaroni Chato

Viongozi na wanachama 51 wa Chadema waliokamatwa jana wakiwa kwenye kikao cha ndani wilayani Chato wanaendelea kushikiliwa na polisi kwa m...




Viongozi na wanachama 51 wa Chadema waliokamatwa jana wakiwa kwenye kikao cha ndani wilayani Chato wanaendelea kushikiliwa na polisi kwa mahojiano.


Miongoni mwa waliotiwa mbaroni wanaoendelea kusota mahabusu ni pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita, Fabian Mahenge na Katibu wake, Sudi Kanganyala.

Mwenyekiti wa Serikali kijiji cha Mkuyuni, Anaclet Twegosora, ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho Kata ya Chato, amewataja viongozi wengine wanaoshikiliwa kuwa ni mwenyekiti wa Baraza la Wazee mkoani Geita, Vitus Makange na Neema Chozaire ambaye ni Mwenyekiti wa Bavicha mkoa.

Wengine ni Kaimu Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Chato, Uhuru Selemani, Katibu wake Mangesai Rudonya na diwani mstaafu kata ya Muganza, Marko Maduka.

Kama ilivyokuwa jana, hakuna kiongozi wa Jeshi la Polisi anayekuwa tayari kulizungumzia suala hili.

Wakati Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, Alex Mkama, ambaye tukio hilo linaendelea wilayani kwake akisema hawezi kulizungumzia, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo, amesema yuko likizo na kuelekeza atafutwe kaimu wake Allan Bukumbi ambaye tangu jana hapokei simu yake ya kiganjani wala kujibu ujumbe mfupi wa maneno anaotumiwa.

Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Ziwa Victoria, Ansbert Ngurumo, amesema kutawanywa kwa mabomu ya machozi na kukamatwa kwa viongozi na wanachama hao ambao walikuwa katika mkutano wa ndani ni kinyume cha sheria kwa sababu vikao vya ndani havihitaji kutoa taarifa wala kibali cha polisi kwa mujibu wa sheria namba 5 ya vyama vya siasa ya mwaka 1995.




COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Wana Chadema 51 mbaroni Chato
Wana Chadema 51 mbaroni Chato
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgt5hDFytsclROCXoQMBgG8T-B_qCHTx2xHA1dxpDzwVv0404Pag8MtSgKi4PihBycf9ENZlp_MlWCqlS8Ldn6ks-n8vfGFCFFKcQo42LposTMTl7KgI0bFQjPRlyMC6RtFO54aaT_s1onu/s640/chadema..jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgt5hDFytsclROCXoQMBgG8T-B_qCHTx2xHA1dxpDzwVv0404Pag8MtSgKi4PihBycf9ENZlp_MlWCqlS8Ldn6ks-n8vfGFCFFKcQo42LposTMTl7KgI0bFQjPRlyMC6RtFO54aaT_s1onu/s72-c/chadema..jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/wana-chadema-51-mbaroni-chato.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/wana-chadema-51-mbaroni-chato.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy