http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Abiria waomba kuruhusiwa kusafiri usiku

Abiria wa mabasi yanayotoka mikoa ya bara yanayopita mkoani Morogoro kuelekea jijini Dar es Salaam wameiomba serikali iruhusu mabasi ya abi...



Abiria wa mabasi yanayotoka mikoa ya bara yanayopita mkoani Morogoro kuelekea jijini Dar es Salaam wameiomba serikali iruhusu mabasi ya abiria kusafiri baada ya saa sita usiku hasa katika maeneo ambayo sio hatarishi kwa usafiri wa wakati huo.


Abiria hao walitoa ombi hilo jana Ijumaa wakati wakizungumza na Mwananchi katika kituo cha mabasi Msamvu.

Wamelalamikia kitendo cha kuzuiwa kuendelea na safari hata kabla ya saa sita usiku na kubainisha kuwa kinasababisha usumbufu mkubwa kwa abiria wengi.

Kwa muda mrefu sasa serikali imepiga marufuku mabasi ya abiria kuendelea na safari baada ya saa sita usiku hivyo baadhi ya mabasi yanayotoka mkoani Mwanza na Mbeya kuelekea Dar es Salaam yanalazimika kulala mkoani Morogoro.

Abiria Shiraji Nyanda alisema kulala njiani kunawaongezea wasafiri gharama na wale wenye watoto wanapata usumbufu zaidi.

"Nia ya serikali ni njema ya kuhakikisha usalama wa watu wake lakini kwa barabara ya Dar-Moro ni salama sana… wangeruhusu tu mabasi yaendelee na safari. Lakini kibaya zaidi tunazuiliwa hapa kabla hata ya hiyo saa sita," alisema Nyanda.

Hata hivyo, kwa mujibu wa kanuni zilizopo, mabasi ya abiria hayaruhusiwi kusafiri baada ya saa nne usiku.

Abiria mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Jane Arnold, ambaye alikua anasafiri na watoto, alisema kulala kwenye basi na watoto kumemsababishia usumbufu na kumuongezea gharama za safari.

Akizungumzia malalamiko hayo, Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani wilaya ya Morogoro, Victor Ayo, alisema mabasi hayo yanazuiliwa Morogoro sit u kwa kuogopa kutenkwa, bali pia kwa usalama wa abiria na vyombo hivyo vya usafiri.

Akifafanua, alibainisha kuwa mabasi yanazuiliwa kusafiri usiku ili pia kupunguza ajali zinazoweza kutokea kutokana na uchovu wa dereva.

Alisema kwa wakati huo dereva anakuwa amechoka baada ya kuendesha gari kwa muda mrefu na barabara hiyo inakuwa na msongamano wa malori.

"Niwashauri tu abiria wawe wavumilivu katika hili kwani linafanyika kulinda usalama wao," alisema.

Ofisa huyo pia aliwataka madereva kutii sheria za usalama barabarani ili kulinda usalama wao na usalama wa watumiaji wengine wa barabara.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Abiria waomba kuruhusiwa kusafiri usiku
Abiria waomba kuruhusiwa kusafiri usiku
http://mobile.mwananchi.co.tz/image/view/-/4006120/medRes/1697355/-/w3b2bg/-/MABASI.jpg?format=xhtml
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/abiria-waomba-kuruhusiwa-kusafiri-usiku.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/07/abiria-waomba-kuruhusiwa-kusafiri-usiku.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy