http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Sumaye aiangukia Serikali, aomba kukivumilia Chadema

Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amefunguka na kuitaka serikali ya awamu ya tano iwavumilie na itambue kuwa Chama Cha Demokrasia na ...


Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amefunguka na kuitaka serikali ya awamu ya tano iwavumilie na itambue kuwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na viongozi wake ni chama halali kinafanya kazi kama CCM inavyofanya kazi zake.


Sumaye aliyasema hayo jana baada ya jeshi la polisi kuzuia msafara wao ambao ulikuwa na lengo la kutembelea na kujionea utendaji kazi wa Manispaa ya Ubungo inayoongozwa na CHADEMA.


"Hili si jambo la ajabu kwa sababu hata viongozi wa CCM kwa mfano hata Pole Pole anazunguka halmshauri zote nchini, ila wanapozunguka wao hakuna tatizo ila inapokuja viongozi wa CHADEMA kidogo tayari wanaanza mapambano, tunadhani huu ni uonevu tu unaendelea wa kujaribu kuwafanya watu wengine wajisikie kwamba hawana uhuru na nchi yao hili nafikiri si jambo jema.


"Serikali tunaomba ituvumilie ijue kwamba CHADEMA pamoja na viongozi wake ni chama halali kinafanya kazi kama CCM wanavyofanya kazi kwa hiyo mambo ya kuandamwa CHADEMA kila mahali inatusikitisha sana" alisema Sumaye


Mbali na hilo Sumaye anasema vitendo hivyo vinavyofanywa kwa viongozi wa CHADEMA ni kutaka kukatisha tamaa jitihada zozote zinazofanywa na viongozi wa chama hicho hivyo anadai ni kitu ambacho hakiwezi kuvumilika.


"Kwa jambo hili mimi nataka tu kuimbia serikali kuwa hawatafanikiwa kwani wataleta vurugu pasipo kuwa na sababu zozote zile, wawaache watu wafanye kazi zao hapa hakuna siasa zozote tunazofanya.

"Tunakagua miradi kwani halimashauri hizi ni zetu kama ambavyo wao wanatembea kwenye halimashauri zote nchini kuona namna Ilani yao inavyotekelezwa na sisi tunataka kujua viongozi wetu wa CHADEMA wanatekeleza vipi yale ambayo CHADEMA imewaagiza kufanya katika Ilani yake. Na miradi hii ni kwa wananchi wote" alisisitiza Sumaye

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Sumaye aiangukia Serikali, aomba kukivumilia Chadema
Sumaye aiangukia Serikali, aomba kukivumilia Chadema
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqK_S5CGXRbCiFiQtxzt0tbIlxqAYNKIGwz5qZW0foByLVc-ImYSFOHiuWCmeUTkAMOgfrsVVpZHtf-SitX-Ql-SlTtsA5_oSZEb_Eqs4qyZZsWqtxwYD_cDLxn9JWPpb2MwO6vv_nstT2/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqK_S5CGXRbCiFiQtxzt0tbIlxqAYNKIGwz5qZW0foByLVc-ImYSFOHiuWCmeUTkAMOgfrsVVpZHtf-SitX-Ql-SlTtsA5_oSZEb_Eqs4qyZZsWqtxwYD_cDLxn9JWPpb2MwO6vv_nstT2/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/sumaye-aiangukia-serikali-aomba.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/sumaye-aiangukia-serikali-aomba.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy