http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Simbachawene Amteua Profesa wa Chuo Kikuu cha UDOM Kuwa Diwani

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amemteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Profesa Davis Mwamfupe ...





Seebait.com 2017
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amemteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Profesa Davis Mwamfupe kuwa diwani katika Manispaa ya Dodoma.


Juzi Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alimtaja Profesa Mwamfupe pamoja na wenzake wawili Roze Nitwa (CCM) na Vicent Tibalindwa (Chadema) kuwa waliteuliwa na Waziri kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo.


Kunambi alisema Simbachawene aliteua majina sita kwa vyama vya Chadema na CCM ndipo wakayapigia kura likiwamo jina la Mwamfupe aliyetokea CCM.


“Waziri alitumia sheria namba 288 (24) (2d) ya Serikali za mitaa na kanuni za uteuzi za mwaka 2010 sura ya 4 (1) na 5 (1) vinavyompa mamlaka ya kufanya hivyo bila kuulizwa na humteua mtu ambaye ni mkazi wa eneo husika,” alisema Kunambi.


Manispaa ya Dodoma haina Meya baada ya Jaffary Mwanyemba kuondolewa na madiwani Machi mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka.


Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alikana madai ya kumwandaa msomi huo wa uchumi katika nafasi ya Umeya ingawa alisema kila mtu mwenye sifa za kuwa diwani ana haki ya kugombea nafasi ya uongozi ikiwamo meya.


Mkurugenzi huyo aliwaondoa hofu waliokuwa wamejenga nyumba zao katika maeneo ambayo hayajapimwa kabla ya kuvunjwa kwa CDA akisema hawatasumbuliwa badala yake watarasimishwa huku akitoa tahadhari kwa wavamizi wa maeneo na viwanja kuwa lazima watavunjiwa.


Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jumanne Ngede alisema baraza la madiwani halina shaka na uteuzi huo na kwamba watapewa ushirikiano katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ikiwamo mchakato wa makao makuu.


Alisema mpango uliopo katika manispaa hiyo ni kujipanga kuwa na ugeni mkubwa ambao umeingia mkoani hapo ikiwemo maofisa wa serikali.


Mmoja wa madiwani ambaye hakupenda kutajwa jina lake alisema mpango wa uteuzi wa msomi huyo unaweza kuwagawa madiwani kwani kuna kila dalili za kuandaliwa kushika kiti hicho huku wengine wakitaka apewe nafasi katika kamati ya uchumi na fedha tu ili akaonyeshe uzoefu wake huko.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amemteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Profesa Davis Mwamfupe kuwa diwani katika Manispaa ya Dodoma.


Juzi Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alimtaja Profesa Mwamfupe pamoja na wenzake wawili Roze Nitwa (CCM) na Vicent Tibalindwa (Chadema) kuwa waliteuliwa na Waziri kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo.


Kunambi alisema Simbachawene aliteua majina sita kwa vyama vya Chadema na CCM ndipo wakayapigia kura likiwamo jina la Mwamfupe aliyetokea CCM.


“Waziri alitumia sheria namba 288 (24) (2d) ya Serikali za mitaa na kanuni za uteuzi za mwaka 2010 sura ya 4 (1) na 5 (1) vinavyompa mamlaka ya kufanya hivyo bila kuulizwa na humteua mtu ambaye ni mkazi wa eneo husika,” alisema Kunambi.


Manispaa ya Dodoma haina Meya baada ya Jaffary Mwanyemba kuondolewa na madiwani Machi mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka.


Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alikana madai ya kumwandaa msomi huo wa uchumi katika nafasi ya Umeya ingawa alisema kila mtu mwenye sifa za kuwa diwani ana haki ya kugombea nafasi ya uongozi ikiwamo meya.


Mkurugenzi huyo aliwaondoa hofu waliokuwa wamejenga nyumba zao katika maeneo ambayo hayajapimwa kabla ya kuvunjwa kwa CDA akisema hawatasumbuliwa badala yake watarasimishwa huku akitoa tahadhari kwa wavamizi wa maeneo na viwanja kuwa lazima watavunjiwa.


Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jumanne Ngede alisema baraza la madiwani halina shaka na uteuzi huo na kwamba watapewa ushirikiano katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ikiwamo mchakato wa makao makuu.


Alisema mpango uliopo katika manispaa hiyo ni kujipanga kuwa na ugeni mkubwa ambao umeingia mkoani hapo ikiwemo maofisa wa serikali.


Mmoja wa madiwani ambaye hakupenda kutajwa jina lake alisema mpango wa uteuzi wa msomi huyo unaweza kuwagawa madiwani kwani kuna kila dalili za kuandaliwa kushika kiti hicho huku wengine wakitaka apewe nafasi katika kamati ya uchumi na fedha tu ili akaonyeshe uzoefu wake huko.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Simbachawene Amteua Profesa wa Chuo Kikuu cha UDOM Kuwa Diwani
Simbachawene Amteua Profesa wa Chuo Kikuu cha UDOM Kuwa Diwani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhKvRkj5gO-FSl7m0AQ1dX77-iMneMNVe_PPzwrjLYpdCH_kIdK9-cKLSsf3xpYbDEtA3k__WXJaFn9ovvsVPUZOWh3WcWNk2LlOlvMIvBfV24UApffMtlUYgfqdigAsmzeD2XxUd3-nzeR/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhKvRkj5gO-FSl7m0AQ1dX77-iMneMNVe_PPzwrjLYpdCH_kIdK9-cKLSsf3xpYbDEtA3k__WXJaFn9ovvsVPUZOWh3WcWNk2LlOlvMIvBfV24UApffMtlUYgfqdigAsmzeD2XxUd3-nzeR/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/simbachawene-amteua-profesa-wa-chuo.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/simbachawene-amteua-profesa-wa-chuo.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy