http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Lowassa aeleza sababu za kutokuvaa sare za CHADEMA

"Si kweli kuwa sivai sare cha CHADEMA, hata nilipokuwa CCM nilikuwa nashona shati la rangi moja ama kijani au njano kisha naweka nem...


"Si kweli kuwa sivai sare cha CHADEMA, hata nilipokuwa CCM nilikuwa nashona shati la rangi moja ama kijani au njano kisha naweka nembo maalumu ya chama, vivyo hivyo hata CHADEMA naweka nembo maalum.


"Na jambo kubwa hapa ni kuwa, nisihukumiwe kwa kuvaa au kutokuvaa sare za CHADEMA lakini kwa matendo yangu."


Hayo ni maneno yaliyotolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa alipokuwa akijibu swali la mtangazaji wa kituo cha Azam Tv, Charles Hillary aliyetaka kujua kwanini havai sare za CHADEMA katika matukio mbalimbali kama ilivyokuwa CCM.


Lowassa alienda mbali na kusema kuwa, sare si jambo kubwa sana kwani mtu anaweza kuvaa sare na bado akawa si mmoja wenu. Unaweza kukuta mtu kavaa nguo za kijani lakini kiukweli moyoni si wa CCM


Aidha, Lowassa alisema, alipomaliza Chuo Kikuu alikwenda jeshini na kwa muda wote huo alikuwa akivaa magwanda, hivyo alishavaa vya kutosha, na umri wake kwa sasa si wa kuvaa tena.


Alipoulizwa kama uamuzi wa kutokuvaa sare ni mbinu ya mwaka 2020 aweze kupata kuungwa mkono na wanachama wa CCM na CHADEMA, alicheka kisha akasema kuwa, kama ni mbinu basi anaamini itafanyakazi.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Lowassa aeleza sababu za kutokuvaa sare za CHADEMA
Lowassa aeleza sababu za kutokuvaa sare za CHADEMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhW406VDjQRoKF1eN0D_ZPb_oN8cWbLsvOL8eZvsLwc05ut45iD8bli2ZIsF5_tFKOJbwlsnWrCYXr0FqjHqxysWPANmURGtyrxSFWclvGT6Rg8q27Yi-U6X3W5iiYYJUzWWhJmpjv1akNA/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhW406VDjQRoKF1eN0D_ZPb_oN8cWbLsvOL8eZvsLwc05ut45iD8bli2ZIsF5_tFKOJbwlsnWrCYXr0FqjHqxysWPANmURGtyrxSFWclvGT6Rg8q27Yi-U6X3W5iiYYJUzWWhJmpjv1akNA/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/lowassa-aeleza-sababu-za-kutokuvaa-sare.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/06/lowassa-aeleza-sababu-za-kutokuvaa-sare.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy