http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mihogo yenye sumu yafyeka uhai wa mtoto Dar

Mtoto wa miaka mitatu amefariki dunia, huku wanafamilia wengine 10 wakinusurika baada ya kula mihogo ya kuchemsha inayosadikiwa kuwa na s...


Mtoto wa miaka mitatu amefariki dunia, huku wanafamilia wengine 10 wakinusurika baada ya kula mihogo ya kuchemsha inayosadikiwa kuwa na sumu.

Tukio hilo lilitokea Mei 19 eneo la Mbondole Manispaa ya Ilala.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbondole, Thomas Nyanduli alisema alipewa taarifa kuwa familia ya Chacha Fyefye yenye watu 11 ilipatiwa matibabu katika zahanati ya Kivule baada ya kula mihogo hiyo.

Nyanduli alisema wengine walihamishiwa Hospitali ya Rufaa Amana ambako baada ya matibabu waliruhusiwa kutokana na afya zao kuimarika.

“Chacha ana watoto tisa pamoja naye na mkewe jumla wapo 11, nilipewa taarifa kuwa siku ya tukio mkewe baada ya kumaliza kuuza mboga eneo la Viwege alinunua mihogo na kwenda nayo nyumbani bila kujua ilikuwa na kitu gani aliipika kwa ajili ya chai.

“Hatuwezi kuthibitisha kama ilikuwa ni sumu ya namna gani, lakini mtoto mmoja amepoteza maisha baada ya kula mihogo hiyo na wengine wameruhusiwa kurejea nyumbani na wanaendelea vizuri,” alisema Nyanduli.

Dereva wa bodaboda, Daud Mseti alisema akiwa kituoni alifuatwa na kutakiwa kwenda nyumbani kwa Chacha kwa ajili ya kuwachukua wagonjwa awapeleke hospitali.

Alisema walipofika nyumbani kwa Chacha, aliwakuta watoto watatu wakiwa wamelazwa chini ambao aliwapakia kwenye pikipiki na kuwapeleka zahanati kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alithibitisha kutokea tukio hilo akisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo. “Juzi nilipata taarifa kuhusu mtoto wa miaka mitatu kufariki dunia akidaiwa kula mihogo yenye sumu na watu wawili ambao mama na mtoto walilazwa katika Hospitali ya Amana,” alisema Hamduni.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mihogo yenye sumu yafyeka uhai wa mtoto Dar
Mihogo yenye sumu yafyeka uhai wa mtoto Dar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_KCujHzIIPw7P6fFbCMaopLl8teu2FoewNjbS0JO0A28gXgkNinefLGsPEZE-VnEYVFcx1e8bquhyphenhyphenAV3GUZeL4XUkH_ybPTt9Y00pYjtbfgyBiHWZ3C1RJYeQ0RL66cXoQ7zvo4I-hJ8D/s640/Cassava-Root.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_KCujHzIIPw7P6fFbCMaopLl8teu2FoewNjbS0JO0A28gXgkNinefLGsPEZE-VnEYVFcx1e8bquhyphenhyphenAV3GUZeL4XUkH_ybPTt9Y00pYjtbfgyBiHWZ3C1RJYeQ0RL66cXoQ7zvo4I-hJ8D/s72-c/Cassava-Root.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/05/mihogo-yenye-sumu-yafyeka-uhai-wa-mtoto.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/05/mihogo-yenye-sumu-yafyeka-uhai-wa-mtoto.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy